tenzi za rohoni

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Tenzi za rohoni

Contents

1 Mwokozi umeokoa. 7

2 Twamsifu Mungu. 8

3 Hata ndimi elfu. 8

4 Jina la Yesu, salamu! 9

5 Jina lake Yesu tamu. 10

6 Baba, Mwana, Roho. 11

7 Ni tabibu wa karibu. 12

8 Taji mvikeni 13

9 Yesu kwetu ni rafiki 13

10 Usinipite! 14

11 Nina haja nawe. 15

12 Ewe Roho wa Mbinguni 16

13 Tafuta daima utakatifu. 17

14 Yesu kwa imani 17

15 Cha kutumaini sina. 18

16 Kumtegemea Mwokozi 19

17 Namwandama Bwana. 20

18 Akifa Yesu nikafa naye. 20

19 Ndiyo dhamana, Yesu wangu. 21

20 Ninaye rafiki naye. 22

21 Roho yangu hima. 23

22 Kale nilitembea. 24

23 Ni salama rohoni mwangu. 25

24 Mwokozi moyoni mwangu. 26

25 Nimekombolewa na Yesu. 27

26 Yesu unipendaye. 28

27 Mungu ni pendo. 29

28 Anipenda ni kweli 29

29 Baba yetu aliye Mbinguni 30

30 Nilikuwa kondoo aliyepotea. 31

31 Msingi imara. 31

32 Yesu awakubali wakosa. 32

33 Dhambi ikikulemea. 33

34 Njoni! Wenye dhambi 34

35 Twende kwake. 35

36 Anisikiaye aliye yote. 35

37 Waitwa, mwovu, na Bwana. 36

38 Twende kwa Yesu. 37

39 Mwenye dhambi huna raha. 37

40 Nasikia kuitwa. 38

41 Yesu aliniita, “Njoo” 39

42 Kivulini mwa Yesu. 40

43 Yesu akwita. 40

44 Kukawa na giza dunia yote. 41

45 Mtazame Huyo aliyeangikwa juu. 42

46 Twae wangu uzima. 43

47 Ni wako wewe. 44

48 Naweka dhambi zangu. 44

49 Nitwae hivi nilivyo. 45

50 Yesu nakupenda, U mali yangu. 46

51 Mungu twatoa shukrani 47

52 Yote namtolea Yesu. 47

53 Wewe umechoka sana. 48

54 Yesu nataka kutakaswa sana. 48

55 Nipe moyo wenye sifa. 49

56 Ni sikukuu siku ile. 50

57 Naendea msalaba. 51

58 Mwamba mwenye imara. 52

59 Peleleza ndani yangu. 53

60 Waponyeni watu. 54

61 Tumesikia mbiu. 54

62 Bwana wa mabwana. 56

63 Ndugu wa kirohoni 57

64 Ujaribiwapo, sifanye dhambi 58

65 Safari 58

66 Po pote mashamba yajaa. 59

67 Bwana uliyewaita. 60

68 Mungu msaada wetu. 61

69 Twendeni askari 62

70 Yesu atuchunga. 62

71 Mteteeni Yesu. 64

72 Twendeni! Haraka! 65

73 Yesu zamani Bethilehemu. 65

74 Wachunga walipolinda. 66

75 Waimba, sikizeni 67

76 Njoni, enyi wa imani 68

77 Msalabani pa Mwokozi 69

78 Sioshwi dhambi zangu. 70

79 Msalaba wa aibu. 71

80 Wamwendea Yesu kwa kusafiwa. 72

81 Chini ya msalaba. 73

82 Sioni haya kwa Bwana. 74

83 Kwa wingi wa nyama. 75

84 Niwonapo mti bora. 75

85 Ni mtu wa simanzi 76

86 Damu imebubujika. 77

87 Deni ya dhambi ilimalizika. 78

88 Ndiyo damu ya Baraka. 79

89 Kwa Kalvari 80

90 Aliteswa, aliteswa. 80

91 Mapenzi yako yafanyike, Bwana. 81

92 Nataka nimjue Yesu. 82

93 Bwana amefufuka. 83

94 Siku ya mbingu kujawa na sifa. 84

95 Hivi vita vimekoma. 85

96 Mle kaburini, Yesu mwokozi 85

97 Tazameni huyo ndiye. 86

98 Huyo ndiye anashuka. 87

99 Maelfu na maelfu. 88

100 Tumrudie Bwana. 89

101 Twonane milele. 90

102 Kazi yangu ikiisha. 90

103 Kaa nami 91

104 Twasoma ni njema sana. 92

105 Kuwatafuta. 93

106 Mungu awe nanyi daima. 94

107 Ewe Baba wa Mbinguni 94

108 Twenenda sayuni 95

109 Nitaimba ya Yesu. 96

110 Mapya ni mapenzi hayo. 97

111 Neno lako Bwana. 98

112 Nilikupa wewe maisha yangu. 99

113 Ni mfalme wa mapenzi 100

114 Bwana Mungu, nashangaa kabisa. 101

115 Kilima kando ya Mji 102

116 Bwana , U sehemu yangu. 103

117 Tufani inapovuma. 103

118 Ni ujumbe wa Bwana. 104

119 Si damu ya nyama. 105

120 Enyi wanadamu. 106

121 Liko lango moja wazi 107

122 Bwana Yesu. 108

123 Nimeketi mimi nili kipofu. 109

124 Mungu ulisema. 109

125 Ati twonane Mtoni?. 110

126 Ni mji mzuri 111

127 Bwana Yesu atakuja. 112

128 Mmoja apita wote. 113

129 Karibu na wewe. 114

130 Niongoze, Bwana Mungu. 115

131 Piga sana vita vyema. 115

132 Sauti sikilizeni 116

133 Ni wako Mungu. 117

134 Juu yake langu shaka. 118

135 Mapenzi ya milele. 119

136 Msifuni, Yesu ndiye mkombozi 120

137 Yesu mponya. 121

138 Tukutendereza Yesu (Luganda) 122

139 Nuru ya rohoni 123

140 Mahali ni pazuri 123

141 Pana jito, lina maji mazuri 124

142 Babangu kule mbiguni. 125

143 Nchi nzuri yametameta. 126

144 Mbele ninaendelea. 126

145 Ndoa yetu nzima. 127

146 Neno la Mungu takata. 128

147 Tegemea mpaka kufa. 129

148 Ondokeni tunaitwa. 130

149 Haya umati wa Yesu. 131

150 Haya ee moyo wangu. 132

151 Usiku mtakatifu. 133

152 Uliyesulibishwa. 134

153 Nimepita  ulimwengu. 135

154 Bariki yote yawe mema. 136

155 Hapana rafiki kama Yesu. 137

156 Bwana Yesu yuko wapi 138

157 Kijito cha utakaso. 139

158 Aniongoza po pote. 139

159 Ushirika mkuu, furaha yangu. 140

160 Jioni moyo wangu wakutafuta. 141

161 Usiku uingiapo. 142

 

 

1 Mwokozi umeokoa

 

1. Mwokozi umeokoa,

Nimekuwa wako wewe.

Damu imenisafisha;

Sifa kwa mwana Kondoo.

 

Utukufu, Aleluya!

Sifa kwa Mwana Kondoo!

Damu imenisafisha,

Utukufu kwa Yesu!

 

2. Nilijitahidi sana

Ila sikupata raha;

Bali kwa kumtegemea

Nilipata Baraka.

 

3. Daima namwegemea

Damu ikifanya kazi,

Nikioga kwa chemichemi

Itokayo Mwokozi.

 

4. Sasa nimewekwa wakfu;

Nitaishi kwako wewe:

Fahari nashuhudia

Ya wokovu wa bure.

 

5. Nasimama kwake Yesu,

Ameponya roho yangu;

Ameniondoa dhambi,

Anifanye mzima.

 

6. Nilikuwa kifungoni,

Niliteswa na dhambi,

Nilifungwa minyororo

Yesu akanifungua.

 

7. Sifa, ameninunua!

Sifa, nguvu za wokovu!

Sifa, Bwana huhifadhi!

Sifa zake milele.

 

2 Twamsifu Mungu

 

1. Twamsifu Mungu kwa Mwana wa Pendo,

Aliyetufia na kupaa juu.

 

Aleluya! Usifiwe; Aleluya! Amin.

Aleluya! Usifiwe, utubariki.

 

2. Twamsifu Mungu kwa Roho Mtukufu,

Ametufunulia Mwokozi wetu.

 

3. Twamsifu Mwana, aliyetufia,

Aliyetwaa dhambi akazifuta.

 

4. Twamsifu Mungu wa neema yote,

Ametukomboa akatuongoza.

 

5. Tuamshe tena, tujazena pendo,

Na moyoni uwashe moto wa Roho.

 

3 Hata ndimi elfu

 

1. Hata ndimi elfu elfu,

Hazitoshi kweli

Bwana Yesu kumsifu,

Kwa zake fadhili.

 

2. Yesu, jina liwezalo

Kufukuza hofu;

Lanifurahisha hilo,

Lanipa wokovu.

 

3. Jina hilo ni uzima;

Ni afya amani;

Laleta habari njema;

Twalipiwa deni.

 

4. Yesu huvunja mapingu

Ya dhambi moyoni;

Msamaha, tena nguvu,

Twapata rohoni.

 

5. Kwa sauti yake vile

Wafu hufufuka

Wakafurahi milele,

Pasipo mashaka.

 

6. Ewe Yesu wangu Bwana,

Uwezo nipewe,

Kuhubiri kote sana,

Wote wakujue.

4 Jina la Yesu, salamu!

 

1. Jina la Yesu, Salamu!

Lisujudieni,

Ninyi Mbinguni, hukumu

Na enzi mpeni.

 

2. Enzi na apewe kwetu,

Watetea dini;

Mkuzeni Bwana wenu,

Na enzi mpeni.

 

3. Enyi mbegu ya rehema,

Nanyi msifuni;

Mmeponywa kwa neema,

Na enzi mpeni.

 

4. Wenye dhambi kumbukeni

Ya msalabani,

Kwa furaha msifuni,

Na enzi mpeni.

 

5. Kila mtu duniani

Msujudieni,

Kote-kote msifuni,

Na enzi mpeni.

 

6. Sisi na wao pamoja

Tu mumo sifani,

Milele sifa ni moja,

Ni “Enzi mpeni.”

5 Jina lake Yesu tamu

 

1. Jina lake Yesu tamu;

Tukilisikia

Hutupoza, tena hamu

Hutuondolea.

 

2. Roho iliyoumia

Kwalo hutibika,

Chakula, njaani pia;

Raha, tukichoka.

 

3. Jina hili ni msingi,

Ngao, ngome, mwamba,

Kwa hili napata wingi,

Kwangu ni akiba.

 

4. Yesu, Mchunga, Rafiki

Mwalimu, Kuhani,

Mwanzo, Mwisho, Njia, Haki,

Uzima kifoni.

 5. Moyo wangu hauwezi,

Kukusifu kweli,

Ila sifa zangu hizi,

Bwana zikubali.

 

6. Na utakaponiita,

Kuja kwako Bwana,

Huko kwako sitaacha

Kukusifu sana.

 

6 Baba, Mwana, Roho

 

1. Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi,

Kila tukiamka tunakuabudu

Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi,

Ewe Utatu, tunakusifu.

 

2. Baba, Mwana, Roho, wakuaminio

Wanakutolea shukrani zao

Wanakusujudia malaika nao:

Wewe u mwanzo, nawe u mwisho.

 

3. Baba, Mwana, Roho, sisi tu gizani,

Utukufu wako hatuoni kosa;

U Mtakatifu, nawe u mapenzi,

U peke yako, mwenzio huna.

 

4. Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi,

Ulivyoviumba vyote vyakusifu:

Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi

Ewe Utatu, tunakusifu.

 

7 Ni tabibu wa karibu

 

1. Ni tabibu wa karibu;

Tabibu wa ajabu;

Na rehema za daima;

Ni dawa yake njema.

 

Imbeni, malaika,

Sifa za Yesu Bwana;

Pweke limetukuka

Jina lake Yesu.

 

2. Hatufai kuwa hai,

Wala hatutumai,

Ila kweli yeye ndiye

Atupumzishaye.

 

3. Dhambi pia na hatia

Ametuchukulia;

Twendeni na amani

Hata kwake Mbinguni.

 

4. Huliona tamu jina

La Yesu Kristo Bwana,

Yuna sifa mwenye kufa

Asishindwe na kufa.

 

5. Kila mume asimame,

Sifa zake zivume;

Wanawake na washike

Kusifu jina lake.

 

6. Na vijana wote tena,

Wapendao sana

Waje kwake wawe wake

Kwa utumishi wake.

 

 

 

 

 

8 Taji mvikeni

 

1. Taji mvikeni,

Taji nyingi tena,

Kondoo mwake kitini,

Bwana wa mabwana;

Name tamsifu

Alikufa kwangu,

Ni mfalme mtukufu,

Mkuu wa Mbingu.

 

2. Taji mvikeni

Mwana wa bikira;

Anazovaa kichwani

Aliteka nyara;

Shiloh wa wanabii,

Mchunga wa watu,

Shina na tanzu vya Yese,

Wa Bethirehemu.

 

3. Taji mvikeni

Bwana wa mapenzi;

Jeraha zake ni shani

Ni vito vya enzi,

Mbinguni hakuna

Hata malaika

Awezaye kuziona

Pasipo kushangaa.

 

9 Yesu kwetu ni rafiki

 

1. Yesu kwetu ni rafiki,

Hwamiwa haja pia;

Tukiomba kwa Babaye

Maombi asikia;

Lakini twajikosesha,

Twajitweka vibaya;

Kwamba tulimwomba Mungu

Dua angesikia.

 

2. Una dhiki na maonjo?

Una mashaka pia.

Haifai kufa moyo,

Dua atasikia

Hakuna mwingine mwema

Wa kutuhurumia;

Atujua tu dhaifu;

Maombi asikia.

 

3. Je, hunayo hata nguvu,

Huwezi kuendelea,

Ujapodharauliwa

Ujaporushwa pia,

Watu wange kudharau,

Wapendao dunia,

Hukwambata mikononi,

Dua atasikia.

 

 

10 Usinipite!

 

1. Usinipite Mwokozi,

Unisikie;

Unapozuru wengine,

Usinipite.

 

Yesu,Yesu,

Unisikie;

Unapozuru wengine,

Usinipite.

 

2. Kiti chako cha rehema,

Nakitazama;

Magoti napiga pale,

Nisamehewe.

 

3. Sina ya kutegemea,

Ila Wewe tu;

Uso wako uwe kwangu;

Nakuabudu.

 

4. U Mfariji peke yako;

Sina Mbinguni,

Wala duniani pote,

Bwana mwingine.

 

11 Nina haja nawe

 

1. Nina haja nawe

Kila saa;

Hawezi mwingine

Kunifaa.

 

Yesu, nakuhitaji

Vivyo kila saa!

Niwezeshe, Mwokozi,

Nakujia.

 

2. Nina haja nawe;

Kaa nami,

Na maonjo haya,

Hayaumi.

 

3. Nina haja nawe;

Kila hali,

Maisha ni bure,

Uli mbali.

4. Nina haja nawe,

Nifundishe

Na ahadi zako

Zifikishe.

 

5. Nina haja nawe,

Mweza yote,

Ni wako kabisa

Siku zote.

 

12 Ewe Roho wa Mbinguni

 

1. Ewe Roho wa Mbinguni

Uje kwetu sasa.

Ufanye makazi yako

Ndani ya Kanisa.

 

2. Ndiwe mwanga, umulike

Tupate jikana;

Mengi kwetu yapunguka,

Tujalize, Bwana.

 

3. Ndiwe Moto, teketeza

Taka zetu zote:

Moyo na iwe sadaka

Ya Mwokozi, yote.

 

4. Ndiwe Umande, na kwako

Tutaburudika,

Nchi kavu itakuwa

Ni yenye Baraka.

 

5. Roho wa Mbinguni uwe

Nasi hapa chini,

Mwili uufananishe

Na kichwa Mbinguni.

13 Tafuta daima utakatifu

 

1. Tafuta daima utakatifu;

Fanya urafiki na Wakristo tu;

Nena siku zotena Bwana wako,

Baraka uombe kwa kila jambo.

 

2. Tafuta daima utakatifu;

Uwe peke yako ukimwabudu;

Ukimwangalia mwokozi wako,

Utabadilishwa kama alivyo.

 

3. Tafuta daima utakatifu;

Kiongozi wako aew Yesu tu;

Katika furaha au huzuni

Dumu kumfuata Yesu Mwokozi.

 

4. Tafuta daima utakatifu;

Umtawaze Roho moyoni mwako;

Akikuongoza katika haki,

Hufanywa tayari kwa kazi yake.

 

 

 

14 Yesu kwa imani

 

1. Yesu kwa imani,

Nakutumaini,

Peke yako;

Nisikie sasa,

Na kunitakasa,

Ni wako kabisa

Tangu leo.

 

2. Nipe nguvu pia

Za kusaidia

Moyo wangu;

Ulikufa wewe,

Wokovu nipewe

Nakupenda wewe,

Bwana wangu.

 

3. Hapa nazunguka

Katika mashaka,

Na matata;

Palipo na giza

Utaniongoza

Hivi nitaweza

Kufuata.

 

4. Takuwa mzima

Nivushe salama

Mautini;

Sina hofu kamwe

Ukiwapo name

Nami nikwandame

Siku zote.

 

 

15 Cha kutumaini sina

 

1. Chakutumaini sina

Ila damu yake Bwana,

Sina wema wa kutosha

Dhambi zangu kuziosha;

 

Kwake Yesu nasimama,

Ndiye mwamba: ni salama

Ndiye mwamba: ni salama.

 

2. Njia yangu iwe ndefu

Yeye hunipa wokovu;

Mawimbi yakinipiga

Nguvu zake ndiyo nanga.

 

3. Damu yake na sadaka

Nategemea daima,

Yote chini yakiisha

Mwokozi atanitosha.

 

4. Nikiitwa hukumuni,

Rohoni nina amani

Nikivikwa haki yake

Sina hofu mbele zake.

 

16 Kumtegemea Mwokozi

 

1. Kumtegemea Mwokozi,

Kwangu tamu kabisa;

Kukubali neno lake

Nina raha moyoni.

 

Yesu,Yesu namwamini,

Nimemwona thabiti;

Yesu,Yesu,yu thamani,

Ahadi zake kweli.

 

2. Kumtegemea Mwokozi,

Kwangu tamu kabisa,

Kuamini damu yake

Nimeoshwa kamili.

 

3. Kumtegemea Mwokozi,

Kwangu tamu kabisa,

Kwake daima napata

Uzima na amani.

 

4. Nafurahi kwa sababu

Nimekutegemea;

Yesu,Mpendwa na Rafiki

Uwe nami dawamu.

 

17 Namwandama Bwana

 

1. Namwndama Bwana kwa alilonena

Njia yangu huning’azia;

Nikimridhisha atanidumisha

Taamini nitii pia.

 

Amini utii, njia pweke ni hii

Ya furaha kwa Yesu: amini ukatii.

 

2. Giza sina kwangu wala hata wingu

Yeye mara huviondoa

Woga, wasiwasi, sononeko, basi;

Huamini nitii pia.

 

3. Masumbuko yote, sikitiko lote;

Kwa mapenzi hunilipia;

Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki

Taamini nitii pia.

 

4. Mimi sitajua raha sawasawa

Ila yote Yesu kumpa;

Napata fadhili na radhi kamili,

Taamini nitii pia.

 

5. Nitamfurahia na kumtumaini,

Majumbani na njia-njia;

Agizo natenda, nikitumwa hwenda,

Huamini nitii pia.

 

18 Akifa Yesu nikafa naye

 

1. Akifa Yesu nikafa naye

Uzima upya huishi naye;

Humtazama mpaka nje:

Nyakati zote ni wake yeye.

 

Nyakati zote nimo pendoni,

Nyakati zote ni uzimani,

Humtazama hata atokee,

Nyakati zote mimi ni wake.

 

2. Vita sipigi visivyo haki,

Na Bwana wangu hapiganiki;

Beramu yake haitwaliki,

Napo po pote hila sitaki.

 

3. Sina mashaka, akawa mbali;

Mizigo yote aihimili;

Ananituliza Imanweli,

Nyakati zote mimi husali.

 

4. Sina huzuni na mimi sidhii;

Simwagi chozi, wala siguni;

Sikuti afa, ila kitini

Daima hunifikiri mimi.

 

5. Kila unyonge huusikia;

Kila ugonjwa kwake hupoa;

Yesu ni mwenye kuniokoa

Nyakati zote hunijalia.

 

 

 

19 Ndiyo dhamana, Yesu wangu

 

1. Ndiyo dhamana, Yesu wangu;

Hunipa furaha za Mbingu;

Mrithi wa wokovu wake

Nimezawa kwa Roho yake.

 

Habari njema, raha yangu

Yesu ndiye Mwokozi wangu,

Habari njema, raha yangu

Yesu ndiye mwokozi wangu.

 

2. Kumsalimu moyo wangu,

Mara namwona raha yangu;

Aniletea malaika,

Wananilinda, taokoka.

 

3. Sina Kinyume, nashukuru,

Mchana kutwa huja kwangu;

Usiku kucha kuna nuru;

Mwokozi wangu; ndimi huru.

 

4. Hali na mali anitwaa!

Mara namwona anifaa,

Nami nangoja kwa subira;

Akiniita, nije mara.

 

 

 

 

20 Ninaye rafiki naye

 

1. Ninaye Rafiki naye

Alinipenda mbele;

Kwa kamba za pendo zake

Nimefungwa milele;

Aukaza moyo wangu,

Uache mageule,

Mimi wake, yeye wangu;

Ndimi naye milele.

                             

2. Ninaye rafiki ndiye

Aliyenifilia;

Alimwaga damu yake

Kwa watu wote pia;

Sina kitu mimi tena,

Nikiwa navyo tele;

Pia vyote ni amana

Ndimi wake milele.

 

3. Ninaye rafiki naye

Uwezo amepewa;

Atanilinda mwenyewe,

Juu tachukuliwa;

Nikitazama Mbinguni,

Hupata nguvu tele;

Sasa natumika chini,

Kisha juu milele.

 

4. Ninaye rafiki naye,

Anao moyo mwema;

Ni mwalimu, kiongozi,

Mlinzi wa daima;

Ni nani wa kunitenga

Na mapenzi ya mbele?

Kwake nimetia nanga,

Ndimi wake milele.

 

21 Roho yangu hima

 

1. Roho yangu hima, na taa yako

Kaiwashe vyema, hapa si pako;

Nguvu zote pia za duniani

Hazitakudhuru ukiamini.

 

Yesu yuko mbele, Yesu yu nyuma,

Yesu vivyo kando, walindwa vyema.

 

2. Adui shetani, na nguvu zake,

Bwana ameshinda, kwa kifo chake;

Wewe nguvu huna, huna kabisa,

Ndiwe mpungufu, mnyonge hasa.

 

3. Toka na mapema, mbele ya wote,

Omba, bisha sana, maisha yote;

Vita vikaliko, macho ukae,

Jivike silaha, nawe sishindwe.

 

4. Bwana Yesu ndiye kwako mchunga,

Neno lake Bwana ndilo upanga;

Mbingu zitakwisha, na nchi pia,

Neno lake Bwana laendelea.

 

22 Kale nilitembea

 

1. Kale nilitembea

Nikilemewa dhambi

Nilikosa msaada,

kuniponya mateso.

 

Usifiwe Msalaba!

Lisifiwe kaburi!

Linalozidi yote,

Asifiwe Mwokozi!

 

2. Hata nilipofika,

Mahali pa Msalaba,

Palinifaa sana,

Sitasahau kamwe.

 

3. Hicho ndicho chanzo,

Cha kufurahi kwangu.

Hapo ndipo mzigo,

Uliponituliwa.

 

4. Panapo msalaba,

Kinatolewa cheti,

Cha kuingia Mbinguni,

Kisicho cha kanisa.

 

5. Yule Bwana mjinga,

Likwenda bila cheti,

Kitumai kwingia,

Kama walio nacho.

 

6. Lipofika langoni,

Akaulizwa cheti,

Cha kumwonyesha Bwana,

Akakutwa hanacho.

 

7. Lituhuzunishalo,

Ni ninyi msio nacho,

Kuwa kama mjinga,

Kwa siku ya arusi!

 

8. Ubavuni mwa Yesu,

Mlitokea damu,

Chemchemi ya uzima,

Itakasayo roho.

 

9. Jitahidi wingie,

Damuni mwa Mwokozi,

Utafutiwa dhambi,

Toka rohoni mwako.

 

23 Ni salama rohoni mwangu

 

1. Nionapo amani kama shwari,

Ama nionapo shida;

Kwa mambo yote umenijulisha,

Ni salama rohoni mwangu.

 

Salama rohoni,

Ni salama rohoni mwangu.

 

2. Ingawa shetani atanitesa,

Nitajipa moyo kwani

Kristo ameona unyonge wangu,

Amekufa kwa roho yangu.

 

3. Dhambi zangu zote, wala si nusu,

Zimewekwa msalabani;

Wala sichukui laana yake,

Ni salama rohoni mwangu.

 

4. Ee Bwana himiza siku ya kuja,

Panda itakapolia;

Utakaposhuka sitaogopa

Ni salama rohoni mwangu.

 

24 Mwokozi moyoni mwangu

 

1. Tangu siku hiyo aliponijia,

Akae moyoni mwangu,

Sina giza tena, ila mwanga pia

Kwa Yesu mwokozi wangu.

 

Amani moyoni mwangu,

kwa Yesu, Mwokozi wangu;

Sina shaka kamwe,

Kwa sababu yeye,

Yu nami moyoni mwangu.

 

2. Sina haja tena, ya kutanga-tanga,

Ndiye kiongozi wangu.

Dhambi zangu zote zimeondolewa,

Na Yesu, Mwanawe Mungu.

 

3. Matumaini yangu ni ya hakika,

Katika Mwokozi wangu.

Hofu zangu na hamu zimeondoka,

kwa kuwa ninaye Yesu.

 

4. Siogopi tena, nikiitwa kufa,

Yu nami daima, Yesu.

Mlango wa Mbinguni ni yeye pia,

“Tapita humo kwa damu.”

 

5. Nitaketi na yeye huko milele,

Nisifu Mwokozi wangu.

Nina raha moyoni majira yote,

Kwa Yesu, Mwanawe Mungu.

 

25 Nimekombolewa na Yesu

 

1. Nimekombolewa na Yesu

Aliyenirehemia;

Kwa bei ya mauti yake

Nimekuwa mtoto wake.

 

Kombolewa!

Nakombolewa na damu;

Kombolewa!

Mimi mwana wake kweli.

 

2. Kukombolewa nafurahi,

Kupita lugha kutamka;

Kulionyesha pendo lake,

Nimekuwa mtoto wake.

 

3. Nitamwona uzuri wake,

Mfalme wangu wa ajabu;

Na sasa najifurahisha,

Katika neema yake.

 

4. Najua taji imewekwa

Mbinguni tayari kwangu;

Muda kitambo atakuja,

Ili alipo, niwepo.

 

26 Yesu unipendaye

 

1. Yesu unipendaye

Kwako nakimbilia,

Ni wewe utoshaye,

Mwovu akinijia;

Yafiche ubavuni,

Mwako maisha yangu;

Nifiikishe mbinguni

Wokoe moyo wangu.

 

2. Ngome nyingine sina;

Nategemea kwako.

Usinitupe Bwana ,

Nipe neema yako,

Ninakuamania

Mwenye kuniwezesha;

Shari wanikingia,

Vitani wanitosha.

 

3. Nakutaka Mpaji

Vyote napata kwako;

Niwapo muhitaji,

Utanijazi vyako;

Nao waangukao

Wanyonge wape nguvu;

Poza wauguao,

Uongoze vipofu.

 

4. Bwana umeniosha

Moyo kwa damu yako;

Neema ya kutosha

Yapatikana kwako;

Kwako Bwana naona

Kisima cha uzima;

Mwangu moyoni Bwana,

Bubujika daima.

 

27 Mungu ni pendo

 

1. Mungu ni pendo, apenda watu;

Mungu ni pendo, anipenda

               

Sikilizeni furaha yangu,

Mungu ni pendo, anipenda.

 

2. Nilipotea katika dhambi,

Nikawa mtumwa wa shetani.

 

3. Akaja Yesu kuniokoa,

Yeye kanipa kuwa huru

 

4. Sababu hii namtumikia,

Namsifu yeye siku zote.

 

28 Anipenda ni kweli

 

1. Anipenda ni kweli;

Mungu anena hili;

Sisi wake watoto;

kutulinda si zito.

 

Yesu anipenda,

Yesu anipenda,

Kweli anipenda,

Mungu amesema.

 

2. Kwa kupenda akafa

Niokoke na kufa;

Atazidi taka,

Sana ataniweka.

 

3. Anipenda kabisa;

Niuguapo sasa

Anitunza Mbinguni

Nniliyelala chini.

 

4. Kunipenda haachi,

Tu sote hapa chini

Baada ya mashaka

Kwake tanipeleka.

 

29 Baba yetu aliye Mbinguni

 

1. Baba yetu aliye Mbinguni

Amenifurahisha yakini

Kuniambia mwake chuoni

Ya kuwa nami Yesu pendoni.

 

Anipenda Mwokozi Yesu,

Anipenda, anipenda;

Anipenda Mwokozi Yesu,

Anipenda mimi.

 

2. Nimuachapo kutanga mbali,

Yeye yu vivyo, hupenda kweli,

Hunirejeza kwake moyoni;

Kweli yu nami Yesu pendoni.

 

3. Anipenda! Nami nampenda;

Kwa wokovu alionitenda;

Akanifia Msalabani

Kwa kuwa nami Yesu pendoni.

 

4. Haya kujua yanipa raha;

Kumuamini kuna furaha;

Humfukuza mara shetani,

Kwona yu nami Yesu Pendoni.

 

5. Sifa ni nyingi asifiwazo,

Moja ni sana katika hizo,

Wala siachi, hata Mbinguni,

Kwimba, “Yu nami Yesu pendoni”.

 

30 Nilikuwa kondoo aliyepotea

 

1. Nilikuwa kondoo aliyepotea,

Sikupenda zizi kamwe, ila kutembea

Nilikuwa mwana asiyesikia,

Sikupenda baba yangu wala kutulia.

 

2. Na mchunga mwema alinitafuta,

Baba kwa mapenzi ndiye aliyenivuta;

Karibu ya kufa, kwa kiu na kwa njaa,

Waliniona mnyonge, waliniokoa.

 

3. Yesu ni mchunga, mwenziwe hapana,

Aliosha taka zangu, dhambi nyingi sana;

Kwa vidonda vyangu alitia dawa.

Ndiye aliyenipata, na kwake nalindwa.

 

4. Nilikuwa kondoo aliyepotea

Sasa nampenda Baba, na mchunga pia;

Kwanza nilitanga na kukosa sana,

Hivi nyumbani mwa Baba sipotei tena.

 

31 Msingi imara

 

1. Msingi imara, enyi wa kweli,

Umekwisha pigwa kwa neno hili;

Aongeze lipi? Mnayo pia

Kwa Yesu mliomkimbilia.

 

2. Wambiwapo vuka maji ya giza,

Mito ya mashaka taipunguza;

Takupa nawe, nikuwezeshe,

Ipata kufaa, isikutishe!

 

3. Utakapopishwa ndani ya moto

Nnguvu nitakupa, upate pato;

Huteketezwi, ila taka zako,

Na zitasalia dhahabu zako.

 

4. Hata zije mvi, walio wangu

Hawaoni kwisha mapenzi yangu;

Nazo zitakapowenea, ndipo

Mabegani mwangu niwatwekapo.

 

5. Na mtu aliyenitegemea

Kamwe kwa adui sitamtia;

Nguvu za jehanam zijapotisha,

Mtu wangu kamwe sitamuacha.

 

32 Yesu awakubali wakosa

 

1. Yesu awakubali,

Wakosa, wahalifu,

Wambieni wa mbali

Habari ya wokovu.

 

Tangazeni kwa bidii,

“Akubali wakosa!”

Liwe neno dhahiri,

“Akubali wakosa!”

 

2. Awakubali Bwana

Neno lake amini

Watu kila aina

Waje kwake tengoni.

 

3. Mimi ni safi moyo

Na mbele ya sharia,

Aliye safi roho

Kwake ilitimia.

 

4. Akubali wakosa;

Nami anikubali;

Alivyonitakasa

Mbinguni niwasili.

 

33 Dhambi ikikulemea

 

1. Dhambi ikikulemea,

Kwa Bwana rehema;

Hivi sasa tegemea

Neno la salama.

 

Tegemea, tegemea,

akwita sasa.

Ni Mwokozi, ni

Mwokozi; amini sasa.

 

2. Yesu amemwaga damu

Ya nyingi baraka;

Nawe sasa oga mumu

Zioshwamo taka.

 

3. Ni njia yeye hakika

Hwongoza rahani;

Usikawe kumshika,

Uwe barakani.

 

4. Karibu nawe wingie

Mwetu safarini,

Twende tukamwamkie,

Milele Mbinguni.

34 Njoni! Wenye dhambi

 

1. Njoni! Njoni! Wenye dhambi,

Njoni, msikawie;

Yesu awangojea ndiye awapendaye;

Ajuaye awezaye

kuwaponya ni Yeye.

 

2. Ewe muhitaji uje;

Anakukaribisha,

Imani, kweli, na toba,

Neema ya kutosha,

Jua sana, kwake Bwana

Bure utapata.

 

3. Njoni, mliolemewa

Na dhambi ya Adamu;

Mkingoja kujiponya

Mtapotea mumu;

Si wa haki, ni wakosa

Waoshwao kwa damu.

 

4. Ikamtokea dhiki,

Mle Gethisemani;

Kisha alipoangikwa

Akalia mtini;

” Imekwisha”, alitosha

Dhabihu ya thamani.

 

5. Kristo aliye Mbinguni

Hutuombea huko;

Basi mtumai yeye;

Kamwe mwingine hako

Yesu pweke, Yesu pweke,

Ndiye Mwokozi wako.

 

6. Wamsifu-sifu sana

Mbinguni malaika;

Wachanganya nyimbo zao

Na waliookoka:

Aleluya wataimba

Waliooshwa taka.

 

35 Twende kwake

 

1. Twende kwake, twende kwake, kwake Yesu sasa,

Sasa twende kwake, kwake Yesu sasa!

 

2. Akwokoe. akwokoe, Bwana Yesu sasa!

Sasa akwokoe, Bwana Yesu, sasa!

 

3. Msadiki, msadiki, Bwana Yesu sasa,

Sasa msadiki, Bwana Yesu sasa!

 

4. Anaweza, anaweza, Bwana Yesu sasa,

Sasa anaweza, Bwana Yesu sasa!

 

5. Anapenda, anapenda, Bwana Yesu, sasa,

Sasa anapenda, Bwana Yesu sasa!

 

6. Njoo hima, njoo hima, kwake Yesu sasa,

Sasa njoo hima, kwake Yesu, sasa!

 

36 Anisikiaye aliye yote

 

1. Anisikiaye, aliye yote;

Sasa litangae, wajue wote,

Duniani kote neno wapate,

Atakaye na aje!

 

Ni “Atakaye”, ni “atakaye”,

Pwani hata bara, na litangae;

Ni Baba Mpenzi alinganaye

Atakaye na aje.

 

2. Anijiliaye, Yesu asema,

Asikawe, aje hima mapema;

Ndimi njia, kweli, ndimi uzima;

Atakaye na aje!

 

3. Atakaye aje, ndivyo ahadi;

Atakaye hiyo, haitarudi!

Atakaye lake, ni la abadi!

Atakaye na aje.

 

37 Waitwa, mwovu, na Bwana

 

1. Waitwa, mwovu, na Bwana

Umwendee hima sana,

Usafiwe dhambi zako,

Humwoni ni mwema kwako?

 

Unaitwa! Itika tu!

Umwendee Bwana Yesu!

Sifiche makosa yako,

Uungame dhambi zako!

Kristo tu umuamini,

Ndiyo njia ua Mbinguni.

 

2. Alilipa damu yake

Ili kukukweza kwake;

Alikufa yeye Bwana,

Mimi nawe tuwe wema.

 

3. Ukifanywa kuwa mwema

Mwishoni utasimama,

Utaingia rahani

Na wapenzi wa zamani.

 

4. Ni mwanga tu, nchi ile;

Uovu hauko kule,

Kwamba wataka ufike

Sharti huku uosheke.

 

38 Twende kwa Yesu

 

1. Twende kwa Yesu mimi nawe,

Njia atwonya tuijue

Imo Chuoni; na Mwenyewe,

Hapa asema, Njoo!

 

Na furaha tutaiona,

Mioyo ikitakata sana,

Kwako, Mwokozi, kuonana,

Na milele kukaa.

 

2. ”Wana na waje”, atwambia,

Furahini mkisikia,

Ndiye mfalme wetu pia,

Na tumtii, Njoo.

 

3. Wangojeani? Leo yupo;

Sikiza sana asemapo;

Huruma zake zikiwapo,

Ewe kijana, Njoo.

 

39 Mwenye dhambi huna raha

 

1. Mwenye dhambi huna raha,

Sikiza nakusihi,

Utapata msamaha

Kwake Yesu Mwokozi!

Njoo hima, njoo hima,

Naye atafurahi.

 

2. Yesu anakwita sana

Naye yuko Mbinguni;

Hofu ya kifo hapana

Kwake ukiamini.

Njoo hima, njoo hima,

Utapata amani.

 

3. Hatakwita siku zote;

Ni ya sasa nafasi.

Lete na uchafu wote,

Kukawa haipasi.

Njoo hima, njoo hima,

Ni wokovu halisi.

 

4. Uzima uko kwa Bwana

Twae uzima hasa

Bure unapatikana,

Wokovu twae sasa!

Njoo hima, njoo hima,

Twae utakatifu.

 

40 Nasikia kuitwa

 

1. Nasikia kwitwa

Na sauti yako

Nikasafiwe kwa damu

Ya kwangikwa kwako.

 

Nimesogea Mtini pako,

Unisafi kwa damu ya kwangikwa kwako.

 

2. Ni mnuonge kweli,

Umenipa nguvu,

Ulivyonisafi taka,

Ni utimilivu.

 

3. Yesu hunijuvya;

Mapenzi, imani;

Tumai, amani, radhi,

Hapa na Mbinguni.

 

4. Huipa imara,

Kazi yake, ndani:

Huongezeka neema,

Ashindwe Shetani.

 

5. Huishuhudia,

Myoyo ya imani

Ya kuzipata ahadi,

Wakimuamini.

 

6. Napata wokovu,

Wema na neema;

kwako Bwana nina nguvu

Na haki daima.

 

41 Yesu aliniita, “Njoo”

 

1. Yesu aliniita, “njoo,

Raha iko kwangu,

Kichwa chako ukilaze

Kifuani mwangu.”

Nilikwenda kwake mara,

Sana nilichoka;

Nikapata kwake raha,

Na furaha tena.

 

2. Yesu aliniita, “njoo,

Kwangu kuna maji,

Maji ya uzima, bure,

Unywe uwe hai, ”

Nilikwenda kwake mara

Na maji nikanywa:

Naishi kwake, na kiu

Kamwe sina tena.

 

3. Yesu aliniita, “njoo,

Dunia ni giza,

Ukinitazama nuru

Takung’arizia.”

Nilikwenda kwake mara

Yeye jua langu,

Ni kila wakati mwanga

Safarini mwangu.

 

42 Kivulini mwa Yesu

 

1. Kivulini mwa Yesu kuna Kituo:

Kituo mbali na hamu, kituo kilicho tamu.

 

Kivulini mwa Yesu kuna kituo;

kivulini mwa Yesu kuna kituo;

Raha tu, mle; amani tupu,

Furaha tele; kivulini mwa Yesu

Raha tu, mle; amani tupu,

Furaha tele; kivulini mwa Yesu.

 

2. Kivulini mwa Yesu nina amani

Iliyopita fahamu, tena itakayodumu.

 

3. Kivulini mwa Yesu, nina furaha;

Furaha yenye fahari, ya kueneza habari.

 

43 Yesu akwita

 

1. Yesu akwita, chanena Chuo:

Uje leo, uje leo;

Kwani kusita? Akwita, Njoo;

Unatanga upeo.

 

Hwita leo, hwita leo.

Yesu akwita kwa upole akwita leo.

 

2. Waliochoka, wapumzike,

Hwita leo, hwita leo:

Wenye mizigo, wakamtweke,

wapate mapumuo.

 

3. Anakungoja, uliye yote,

Uje leo, uje leo;

Uliyekosa usijifiche:

Woshwe, uvikwe nguo.

 

4. Yesu asihi wakawiao,

Waje leo, waje leo.

Watafurahi waaminio;

Usije kwani? Njoo.

44 Kukawa na giza dunia yote

 

1. Kukawa na giza dunia yote,

Ni Mwanga wa ulimwengu,

Ikaisha ulipokuja yote,

Ni mwanga wa ulimwengu.

 

Jua, Yesu hana mwenziwe!

Nalipofuka kama wewe:

Nakuombea umwone nawe,

Ni mwanga wa ulimwengu.

 

2. Hatuna giza tudumuo mwake,

Ni mwanga wa ulimwengu;

Tumwandamiapo nyayoni mwake

Ni mwanga wa ulimwengu.

 

3. Enyi wa gizani wenye kutanga!

Ni mwanga wa ulimwengu,

Kaulekeeni, mpate lenga;

Ni mwanga wa ulimwengu.

 

4. Tutamwona Mwokozi juu ya mbingu

Ni mwanga wa ulimwengu:

Ni nuru za mbingu kondoo wa Mungu

Ni mwanga wa ulimwengu.

 

45 Mtazame Huyo aliyeangikwa juu

 

1. Mtazame Huyo! Aliyeangikwa juu

Hivi sasa upate ishi.

Mwenye – dhambi dhaifu, mtazame tu

Wala usifanye tashwishi.

 

Tazama! Tazama! Tazama uishi!

Mtazame huyo aliyeangikwa juu

Hivi sasa upate ishi.

 

2. Kama mwana kondoo hakuondoa dhambi,

Na makosa yako maovu!

Kama deni zetu zote hakulipa

Mbona imemwagika damu?

 

3. Si kutubu na sala ikomboayo,

Ila damu ndiyo salama;

Na aliyeimwaga aweza, sasa,

Dhambi zako kukufutia.

 

4. Usiwe na shaka, Mungu amesema,

Hakuna alilolisaza;

Hapo alipokuja alitimiza

Kazi zote alizoanza.

 

5. Basi twae uzima, kwa kufurahi

Upokee kwa Bwana, sasa;

Ujijue hakika kwake kuishi

Yesu aishiye kabisa.

 

46 Twae wangu uzima

 

1. Twae wangu uzima,

Sadaka ya daima;

Twae saa na siku,

Zikutukuze huku.

 

2. Twae mikono nayo

Ifanye upendavyo,

Twae yangu miguu

Kwa wongozi wako tu.

 

3. Twae sauti yangu,

Niimbe kwa Mungu tu;

Itwae na midomo,

Ijae neno lako.

 

4. Twae dhanabu pia,

Na yote ya dunia;

Twae yangu hekima,

Upendavyo tumia.

 

5. Nia itwae, Mungu,

Haitakuwa yangu;

Twae moyo; ni wako,

Uwe makazi yako.

 

6. Twae mapenzi yangu,

Sifa za moyo wangu;

Twae kabisa nafsi

Nniwe wako halisi.

 

47 Ni wako wewe

 

1. Ni wako wewe, nimekujua,

Na umeniambia;

Lakini Bwana, nataka kwako nizidi kusongea.

 

Bwana vuta, vuta, nije nisongee,

Sana, kwako mtini.

Bwana vuta, vuta, nije nisongee,

Pia damu ya thamani.

 

2. Niweke sasa nikatumike

Kwa nguvu za neema;

Uyapendayo nami nipende,

Nizidi kukwandama.

 

3. Nina furaha tele kila saa

Nizungumzavyo kwako,

Nikuombapo nami napata kujua nia yako.

 

4. Mapenzi yako hayapimiki,

Ila ng’ambo ya liko.

Anasa pia sitazijua,

Bila kufika kwako.

 

48 Naweka dhambi zangu

 

1. Naweka dhambi zangu

Juu yake Bwana

Kuziondoa, kwangu

Hulemea sana;

Na uaili wangu

Ameuondoa;

Dawa yangu ni damu,

Kwa hiyo napoa.

 

2. Na uhitaji wangu

Nitamjuvisha

Kwa upungufu wangu

Yeye anatosha;

Majonzi yangu yote

Na mizigo yangu,

Atachukua vyote

Yesu Bwana wangu.

 

3. Na roho yangu nayo,

Imechoka sana;

Namletea hiyo

Ilindwe na Bwana;

Ni jema jina lake,

Nalo lapendeza,

Imanweli na kwake

tutalitukuza.

 

4. Natamani daima

Niwe kama Bwana,

Mpole, tena mwema,

Wa mapenzi sana;

Zaidi natamani

Kwenda kwake juu,

Nikaone mbinguni

Enzi yake kuu.

49 Nitwae hivi nilivyo

 

1. Nitwae hivi nilivyo,

Umemwaga damu yako,

Nawe ulivyoniita,

Bwana Yesu,naja,naja.

 

2. Hivi nilivyo;si langu

Kujiosha roho yangu;

Nisamehe dhambi zangu,

Bwana Yesu,naja,naja.

 

3. Hivi nilivyo; sioni

Kamwe furaha moyoni;

Daima ni mashakani,

Bwana Yesu,naja,naja.

 

4. Hivi nilivyo kipofu,

maskini na mpungufu;

Wewe u mtimilifu;

Bwana Yesu,naja,naja.

 

5. Nawe hivi utanitwaa;

Nisithubutu kukawa,

Na wewe hutanikataa,

Bwana Yesu,naja,naja.

 

6. Hivi nilivyo;mapenzi

Yamenipa njia wazi;

Hali na mali sisazi,

Bwana Yesu,naja,naja.

 

50 Yesu nakupenda, U mali yangu

 

1. Yesu nakupenda, U mali yangu,

Anasa za dhambi sitaki kwangu;

Na Mwokozi aliyeniokoa,

Sasa nakupenda, kuzidi pia.

 

2. Moyo umejaa mapenzi tele

Kwa vile ulivyonipenda mbele,

Uhai wako ukanitolea

Sasa nakupenda, kuzidi pia.

 

3. Ulipoangikwa Msalabani

Tusamehewe tulio dhambini;

Taji ya miiba uliyoivaa,

Sasa nakupenda, kuzidi pia.

 

4. Niwapo hai, niwapo maiti,

Kupendana nawe kamwe siachi;

Hari za kifo zikinienea,

Sasa nakupenda, kuzidi pia.

 

5. Mawanda mazuri, na masikani

Niyatazamapo huko Mbinguni,

Tasema na taji nitakayovaa

Sasa nakupenda, kuzidi pia.

 

51 Mungu twatoa shukrani

 

Mungu twatoa shukrani,

Kwa kutulinda usikuni,

Na kutuangalia mchana,

Kutuongoza kila mara.

 

52 Yote namtolea Yesu

 

1. Yote namtolea Yesu

Nampa moyo wote,

Nitampenda siku zote,

Namwandama kila saa.

 

Yote kwa Yesu,

Yote kwa Yesu,

Yote kwako, Ee mwokozi,

Natoa sasa.

 

2. Yote namtolea Yesu,

Nainamia pake;

Nimeacha na anasa,

Kwako Yesu nipokee,

 

3. Yote namtolea Yesu,

Nifanye niwe wako;

Nipe Roho yako, Bwana,

Anilinde daima,

 

4. Yote namtolea Yesu,

Nami naona sasa;

Furaha ya ukombozi,

Nasifu jina lake,

 

53 Wewe umechoka sana

 

1. Wewe umechoka sana?

Wataka raha?

Kwake Yesu utapata furaha.

 

2. Alama anazo yeye?

Sasa! makovu ya mikono, na miguu,

Na mbavu.

 

3. Nacho kimivukwa taji

Kichwa cha huba?

Alivikwa taji kweli miiba.

 

4. Huku nikimfuata nipate nini?

Maonjo nje na ndani amani.

 

5. Kwamba namwandama Bwana,

Mwisho ni nini?

Ni furaha na salama

Mbinguni.

 

54 Yesu nataka kutakaswa sana

 

1. Yesu nataka kutakaswa sana,

Nataka moyo uwe enzi yako.

Ukiangushe kilichoinuka

Unioshe sasa niwe mweupe.

 

Mweupe tu, ndiyo mweupe,

Ukiniosha nitakuwa safi.

 

2. Bwaba Yesu, unitazame sasa,

Unifanye niwe dhabihu hai;

Najitoa kwako, na moyo wote;

Unioshe sasa niwe mweupe.

 

3. Bwana kwa hiyo nakuomba sana,

Nakungojea miguuni pako,

Naomba unioshe damuni tu,

Unioshe sasa niwe mweupe.

 

4. Bwana nidumu kukungojea,

Niumbie moyo safi, Ee Mungu,

Wanaokujia hutupi kamwe,

Unioshe sasa niwe mweupe.

 

55 Nipe moyo wenye sifa

 

1. Nipe moyo wenye sifa

Sio wa utumwa;

Moyo ulionyunyizwa

Damu ya thamani.

 

2. Moyo msikizi, moyo

Wa kunyenyekea,

Moyo utawaliwao

Na Mwokozi pia.

 

3. Mwenye kutubu, mnyonge,

Sadiki, amini;

Kamwe, kamwe asitengwe

Akaaye ndani.

 

4. Mpya, mwema na mawazo

Mwingi wa mapenzi

Nawe uwe kielelezo

Moyo wa Mwokozi.

 

5. Ni uule moyo wako;

Moyo wa huruma

Yesu, natamani kwako

Kukujua vyema.

 

6. Na ya midomo matunda

Yako, nipe nami;

Amani isiyokoma

Iwe yangu mimi.

 

7. Nitie yako tabia,

Inishukie juu;

Jina lako nipe pia,

Ndilo la upendo.

 

8. Ni wa baba utukufu;

Mwana atukuke;

Na roho Mtakatifu

U utatu pweke.

 

 

56 Ni sikukuu siku ile

 

1. Ni siku kuu siku ile

Ya kumkiri Mwokozi!

Moyo umejaa tele,

Kunyamaza hauwezi.

 

Siku kuu! Siku kuu!

Ya kuoshwa dambi zangu kuu!

Hukesha na kuomba tu,

Ananiongoza miguu.

Siku kuu! siku kuu!

Ya kuoshwa dhambi zangu kuu.

 

2. Tumekwisha kupatana

Mimi wake, yeye wangu,

Na sasa nitamwandama,

Nikiri neno la Mungu.

 

3. Moyo tulia kwa Bwana

Kiini cha raha yako,

Huna njia mbili tena;

Yesu ndiye njia yako.

 

4. Nadhiri yangu ya mbele

Nitaiweka daima,

Hata ije siku ile,

Ya kwonana kwa salama

 

57 Naendea msalaba

 

1. Naendea Msalaba,

Ni mnyonge na mpofu,

Yapitayo naacha,

Nipone Msalabani.

 

Nakutumaini tu,

Ewe Mwana wa Mungu;

Nainamia kwako;

Niponye, mponya wangu.

 

2. Nakulilia sana:

Nalemewa na dhambi;

Pole Yesu asema;

“Nitazifuta zote”.

 

3. Natoa vyote kwako,

Nafasi nazo nguvu,

Roho yangu na mwili,

Viwe vyako milele.

 

4. Kwa damu yake sasa,

Nimegeuka roho,

Nikaziacha tama

Nimfuate Yesu tu.

 

5. Yesu yuaja tena!

Nimepevuka kwake,

Kila chembe kamili;

Msifuni yeye mponya!

 

58 Mwamba mwenye imara

 

1. Mwamba wenye imara

Kwako nitajificha!

Maji hayo na damu

Yaliyotoka humu,

Hunisafi na dhambi,

Hunifanya mshindi.

 

2. Kwa kazi zote pia ,

Sitimizi sharia.

Nijapofanya bidii,

Nikilia nakudhii,

Hayaishi makosa;

Ndiwe wa kuokoa.

 

3. Sina cha mkononi,

Naja Msalabani;

Nili tupu, nivike;

Ni mnyonge, nishike;

Nili mchafu naja,

Nioshe nisijafa.

 

4. Nikungojapo chini,

Nakwenda kaburini;

Nipaapo Mbinguni,

Na kukwona enzini:

Roho yangu na iwe

Rahani mwako wewe.

 

59 Peleleza ndani yangu

 

1. Peleleza ndani yangu,

Iwe safi nia,

Kwangu kama kwako Mungu,

Idhihiri pia.

 

2. Peleleza moyo wangu

Uunifunulie,

Yaliyomo ndani yangu

Nami niyajue.

 

3. Kwanza washe zako tambi,

Kumefunga giza;

Nijue ambavyo dhambi

Ni la kuchukiza.

 

4. Peleleza na mawazo

Ni mbegu za mambo,

Asili ya machukizo,

Maumbuo – umbo.

 

5. Zidi kuyapeleleza

Katikati yangu

Hata wishe nifundisha

Udhaifu wangu.

 

6. Hapo nikikwinamia

Mbele zako, Mungu,

Hakika nitakujua

U mpenzi wangu.

 

60 Waponyeni watu

 

1. Waponyeni watu wamo kifoni,

Watoeni walio shimoni;

Na aangukaye mumzuie;

Ya Bwana Yesu wahubirini.

 

Walio kifoni waokoeni,

Mwokozi yuko, wahubirini.

 

2. Wajapokawia anangojea,

Awasubiri waje tobani;

Msiwadharau, muwaonyeni;

Huwasamehe; wakiamini.

 

3. Myoyoni mwa ndani, yule shetani

Ameyaseta mawazo yao;

Lakini kwa Bwana huwa mazima,

Tukiwavuta kwa pole hao.

 

4. Kawaokoeni, wale njiani,

Mutimize mapenzi ya Bwana;

Na kwa nguvu zake warudi kwake,

Kwa subira waonyeni sana.

 

61 Tumesikia mbiu

 

1. Tumesikia mbiu:

Yesu lo! aponya,

Utangazeni kote,

Yesu, lo! aponya.

Tiini amri hiyo;

Nchini na baharini,

Enezeni mbiu hii;

Yesu , lo! aponya.

 

2. Imbeni na vitani;

Yesu, lo! aponya;

Kwa nguvu ya kombozi,

Yesu, lo! aponya.

Imbeni wenye shida,

Unapoumwa moyo.

Na karibuni imba;

Yesu, lo! aponya.

 

3. Mawimbini uenee;

Yesu, lo! Aponya;

Wenye dhambi jueni;

Yesu, lo! Aponya.

Visiwa na viimbe,

Vilindi itikeni,

Na nchi shangilieni;

Yesu, lo! Aponya.

 

4. Upepo utangaze;

Yesu, lo! Aponya;

Mataifa yashangaaa;

Yesu lo! Aponya.

Milimani, bondeni,

Sauti isikike

Ya wimbo wa ushindi;

Yesu, lo! Aponya.

 

62 Bwana wa mabwana

 

1. Bwana wa mabwana,

Mwenye nguvu sana

Twakusihi:

Neno la milele

Na liende mbele,

Waongoke tele

Kwa Mwokozi.

 

2. Tunaowaona

Wanavyopatana,

Kulipinga,

Hawataliweza

Neno, kulitweza:

Huwaje! Kucheza:

Na upanga?

 

3. Heri wajitunze

Ili wapatane,

Na Mwokozi;

Watafute sana,

Wapate kuona,

Yesu kuwa Bwana,

Mkombozi.

 

4. Mungu awaita

Wasije kukuta

Pigo lake;

Hakuona vyema

Wakose uzima,

Awape rehema,

Waokoke.

 

5. Mwenye utukufu

Tunamshukuru

Yeye pweke!

Nasifiwe sana,

Baba, naye Mwana,

Na wa tatu tena

Roho yake.

 

63 Ndugu wa kirohoni

 

1. Ndugu wa kirohoni

Mliokombolewa,

Tafakarini sana

Yatupasayo.

 

Wapenzi wake Yesu

Tuliokombolewa

Tujitoe kabisa

Wengi waponywe.

 

2. Siku itatimia

Tutakapoulizwa

Wale wa nyumba zetu

Na majirani

 

3. Tujitoeni, ndugu,

Tukahubiri Injili.

Atutumie Roho

kuponya wengi.

 

4. Wasiokombolewa

Ni wengi vijijini,

Wataokolewaje

Tukiogopa?

 

5. Bwana alijitoa

Akapotewa mengi,

Ili atuokoe,

Tusiwe waoga.

 

6. Aliyetununua,

Kwa kuimwaga damu,

Angalieni sana

Msimwepuke.

 

64 Ujaribiwapo, sifanye dhambi

 

1. Ujaribiwapo, sifanye dhambi,

Bali uzishinde, kwa Yesu kutii.

Fuliza kiume ushinde tamaa;

Yesu ni Mwokozi, hukuokoa.

 

Umwombapo yu papo

Akuongeze nguvu,

Atakusaidia;

Yesu atakufaa.

 

2. Wepushe waovu, matusi dharau;

Heshima la Mungu, kamwe sisahau;

Fanya uhodari, uwe mpole,

Atakuokoa hata milele.

 

3. Avumiliaye hupewa taji;

Tujaposumbuka tu washindaji,

Na mwokozi wetu hutuwezesha

Tusiwe kushindwa kama twakesha.

 

65 Safari

 

1. Katika safari yetu

Kwenda Mbinguni

Tusiishe siku zetu

Usingizini.

 

Ng’oani! Tujifungeni,

Twende zetu juu!

Kristo ndiye kiongozi;

Tusihofu tu.

 

2. Atwekwe badala yetu,

Mwenyewe Bwana;

Yesu kiongozi wetu

Atapokea.

 

3. Kisimani, maji tele,

Maji mazima!

Maji hayo,

Ya milele

Yana neema.

 

4. Njiani miiba mingi,

Yatuumiza;

Hofu na hatari nyingi,

Sana zakaza.

 

5. Kweli, njia ya Mbinguni

Ni ya mashaka;

Tuwe na Yesu njiani,

Mara hufika.

 

66 Po pote mashamba yajaa

 

1. Po pote mashamba yajaa,

Tele nafaka pevu,

Po pote yang’aa meupe

Bondeni na nyandani.

 

Mwenye mavuno, wasihi

Upeleke wavuni,

Wakusanye mazao,

Hata kazi iishe.

 

2. Wapeleke uchaoni,

Waende na jotoni,

Mpaka jua lishukapo

Wakusanye ko kote.

 

3. Watenda kazi wa Bwana,

Mlete sasa mazao,

Na jioni ingieni

Kwake na furaha kuu.

 

67 Bwana uliyewaita

 

1. Bwana uliyewaita

Watakatifu wako,

Wawe mitume, wachunga,

Walishe kundi lako;

wanyonge na wenye hofu

Wakawa mashujaa,

Na wapole wa kunena

Wasiwe kunyamaa.

 

2. Hata leo wawataka

Watakatifu wako,

Nawe wauliza tena

Ni nani aliyeko

Atakaye nimtume

Afundishe vijana?

“Ni tayari, Bwana wangu,

Nitume mimi Bwana.”

 

3. Nitume na mimi, Bwana

Kama ulivyotumwa,

Habari ya msamaha

Na dhambi kutubiwa,

Niwahubiri wakosa,

Na waliopotea,

Wokovu u wake Bwana,

Aliyewafilia.

 

4. Astahiliye hapana

Kutamka habari,

Lakini wewe waweza

Kutufanya tayari.

Neno lako tulijue,

Tupe na roho yako,

Hayatakuwa ya bure,

Haya maneno yako.

 

68 Mungu msaada wetu

 

1. Mungu msaada wetu

Tangu myaka yote,

Ndiwe tumaini letu

La zamani zote.

 

2. Kivuli cha kiti chako

Ndiyo ngome yetu.

Watosha mkono wako

Ni ulinzi wetu.

 

3. Kwanza havijakuwako

Nchi na milima,

Ndiwe Mungu; chini yako

Twakaa salama.

 

4. Na myaka elfu ni kama

Siku moja kwako;

Utanilinda daima

Tu wenyeji wako.

 

5. Binadamu huondoka,

Mwisho hana kitu;

Kama ndoto hutoweka

Ndivyo hali yetu.

 

6. Ila wewe Mungu wetu

Ndiwe wa kudumu;

Ndiwe bora, ngome yetu

Twakaa dawamu.

 

69 Twendeni askari

 

1. Twendeni askari, watu wa Mungu;

Yesu yuko mbele, tumwandame juu.

Ametangulia Bwana vitani,

Twende mbele kwani ndiye amini.

 

Twende askari watu wa Mungu;

Yesu yuko Mbele, tumwandame juu.

 

2. Jeshi la Shetani, likisikia

Jina la Mwokozi, litakimbia,

Kelele za shangwe zivume nchi;

Ndugu inueni zenu sauti.

 

3. Kweli kundi dogo, watu wa Mungu

Sisi na mababa tu moja fungu.

Hatutengwi nao, moja imani,

Tumaini moja, na moja dini.

 

4. Haya mbele watu nasi njiani,

Inueni myoyo, nanyi sifuni;

Heshima na sifa ni ya Mfalme,

Juu hata chini, sana zivume.

 

70 Yesu atuchunga

 

1. Yesu atuchunga,

Mchunga wetu,

Naye atufuta

Machozi yetu;

Mkononi mwake

Hatuna hofu,

Daima twapata

Kwake wokovu.

 

2. Yesu atuchunga

Tumemjua,

Na sauti yake

Twaitambua;

Naye akituonya

Ni kwa upole,

Tu kondoo zake

Hata milele.

 

3. Yesu atuchunga;

Aliwafia

Kondoo wakubwa

Na wana pia;

Kwamba awajua,

Kondoo zake,

Hutiwa alama

Ya damu yake.

 

4. Yesu atuchunga;

Mikono yake

Imewaambata

Kondoo zake;

Hapati wadhuru

Adui yule,

Yesu awalinda.

 

71 Mteteeni Yesu

 

1. Mteteeni Yesu,

Mlio askari;

Inueni beramu,

Mukae tayari,

Kwenda nae vitani,

Sisi hatuchoki

Hata washindwe pia

Yeye amiliki.

 

2. Mteteeni Yesu,

Vita ni vikali;

Leo siku ya Bwana,

Atashinda kweli,

Waume twende naye,

Adui ni wengi,

Lakini kwake Bwana

Tuna nguvu nyingi.

 

3. Mteteeni Yesu,

Wenye ushujaa;

Nguvu zenu za mwili

Hazitatufaa;

Silaha ya injili

Vaeni daima,

Kesheni mkiomba,

Sirudini nyuma.

 

4. Mteteeni Yesu,

Vita ni vikali,

Wengi wamdharau,

Hawamkubali,

Ila atamiliki

Tusitie shaka,

Kuwa naye vitani

Twashinda hakika.

 

72 Twendeni! Haraka!

 

1. Twendeni! Haraka! Tupeleke Neno

Liwe mwanga kwa nchi zilizo giza.

Bwana alisema nendeni po pote

Kawafundisheni mataifa yote.

Pelekeni Injili kwa jina la Yesu.

Upesi! Twendeni haraka!

 

2. Twendeni! Haraka! Tupeleke Neno

La upendo wa Mungu kwa watu wote;

Aliyeupenda sana ulimwengu

Akamtoa Yesu Mwana wake pekee

Kaleta wokovu, tumtangazeni.

Upesi! Twendeni haraka!

 

3. Twendeni! Haraka! Tupeleke Neno

La uzima kwa watu waliokufa.

Mateka ya Shetani litafungua

Litaponyesha na kuwapa amani.

Twendeni upesi, tukawaokoe.

Upesi! Twendeni haraka!

 

73 Yesu zamani Bethilehemu

 

1. Yesu zama Bethilehemu,

Aliyezaliwa kwa aibu,

Ndiye mwakozi wa ulimwengu,

Akaja kwa mimi.

 

Akaja kwa mimi; akaja kwa mimi;

Ndiye mwaokozi wa ulimwengu,

Akaja kwa mimi.

 

2. Yesu akafa msalabani,

Kuniponya akalipa deni,

Ni la ajabu ya jinsi gani

Kunifia mimi!

 

Kunifia mimi! Kunifia mimi!

Ni la ajabu ya jinsi gani

Kunifia mimi.

 

3. Ni yeye huyo tangu asili;

Na nilipotanga-tanga mbali

Alikuja kwa upole, kweli

Kuniita mimi.

 

Kuniita mimi; Kuniita mimi;

Alikuja kwa upole, kweli

Kuniita mimi

 

4. Yesu kristo atarudi tena,

Hilo lanifurahisha sana.

Yeye Bwana akionekana

Kunijia mimi.

 

Kunijia mimi, kunijia mimi,

Yeye Bwana akionekana

Kunijia mimi

 

74 Wachunga walipolinda

 

1. Wachunga walipolinda

Kucha nyama zao,

Malaika mtukufu

Alishuka kwao.

 

2. Wakacha sana wachunga,

Akawatuliza,

“Nawaletea habari

Ya kuwapendeza.”

 

3. ”Mji ule wa Daudi

Leo amezawa

Mwokozi ni Kristo Bwana,

Ilivyoandikwa”.

 

4. ”Huyo mwana wa Mbinguni

Ataonekana,

Amelazwa kihorini

Malazi hapana.”

 

5. Alipokwisha yanena

Malaika hao

Waliimba wimbo huu

Usio na mwisho:

 

6. ”Enzi ni yake Munju juu,

Na nchi salama,

Kwa watu nao radhi kuu,

Sasa na daima.”

 

75 Waimba, sikizeni

 

1. Waimba, sikizeni,

Malaika Mbinguni;

Wimbo wa tamu sana

Wa pendo zake Bwana,

“Duniani salama,

Kwa wakosa rehema.”

Sisi sote na twimbe

Nao wale wajumbe;

Waimba, sikizeni,

Malaika mbinguni.

 

2. Ndiye Bwana wa Mbingu,

Tangu milele Mungu,

Amezaliwa mwili,

Mwana wa mwanamwali;

Ametoka enzini

Kuja ulimwenguni

Mwokozi atufie,

Ili tusipotee.

Waimba, sikizeni,

Malaika Mbinguni.

 

3. Mtukufu wa amani

Ametoka Mbinguni,

Jua la haki, ndiye

Atumulikiaye;

Amejivua enzi,

Alivyo na mapenzi,

Ataka kutuponya,

Kutuzalisha upya,

Waimba sikizeni,

Malaika Mbinguni.

 

4. Njoo upesi, Bwana,

Twakutamani sana;

Kaa nasi, mwokozi

Vita hatuviwezi;

Vunja kichwa cha nyoka,

Sura zako andika,

Tufanane na wewe,

Kwetu sifa upewe,

Waimba, sikizeni,

Malaika Mbinguni.

 …

76 Njoni, enyi wa imani

 

1. Njoni na furaha, enyi wa imani,

Njoni Bethilehemu upesi !

Amezaliwa jumbe wa Mbinguni;

Njoni tumuabudu, njonu tumuabudu,

Njoni tumuabudu Mwokozi.

 

2. Mungu wa waungu, Mwanga wa mianga,

Amekuwa radhi kuzaliwa;

Mungu wa kweli, wala si kiumbe;

Njoni tumuabudu, njonu tumuabudu,

Njoni tumuabudu Mwokozi.

 

3. Jeshi la Mbinguni, Imbeni kwa nguvu,

Mbingu zote na zijae sifa;

Sifuni Mungu aliye Mbinguni;

Njoni tumuabudu, njonu tumuabudu,

Njoni tumuabudu Mwokozi.

 

4. Ewe Bwana mwema, twakubarikia,

Yesu, utukufu uwe wako;

Neno la Baba limekuwa mwili;

Njoni tumuabudu, njonu tumuabudu,

Njoni tumuabudu Mwokozi.

 

77 Msalabani pa Mwokozi

 

1. Msalabani pa mwokozi,

Hapo niliomba upozi,

Akaniokoa mpenzi,

Mwana wa Mungu.

 

Mwana wa Mungu, Mwokozi wangu,

Akaniokoa mpenzi, Mwana wa Mungu.

 

2. Chini ya mti msumbufu,

Niliomba utakatifu,

Alinikomboa kwa damu,

Mwana wa Mungu.

 

Mwana wa Mungu, Mwokozi wangu,

Alinikomboa kwa damu, Mwana wa Mungu.

 

3. Aliniokoa dhambini,

Ikawa kunikaa ndani,

Aliponifia mtini,

Mwana wa Mungu.

 

Mwana wa Mungu, Mwokozi wangu,

Aliponifia Mtini, Mwana wa Mungu.

 

4. Damu ya Yesu ya thamani,

Huniokoa makosani,

Huniendesha wokovuni,

Mwana wa Mungu.

 

Mwana wa Mungu, Mwokozi wangu,

Huniendesha wokovuni, Mwana wa Mungu.

 

5. Hicho kijito cha gharama,

Leo jivike kwa kuzama,

Kwake uuone uzima,

Mwana wa Mungu.

 

Mwana wa Mungu, Mwokozi wangu,

Kwake uu…

78 Sioshwi dhambi zangu

 

1. Sioshwi dhambi zangu,

Bila damu yake Yesu.

Hapendezewi Mungu,

Bila damu yake Yesu.

 

Hakuna kabisa

Dawa ya makosa

Ya kututakasa,

Ila damu yake Yesu.

 

2. La kunisafi sina

Ila damu yake Yesu.

Wala udhuru tena,

Ila damu yake Yesu.

 

3. Sipati pataniswa,

Bila damu yake Yesu.

Hukumu yanitisha,

Bila damu yake Yesu.

 

4. Sipati tumaini,

Bila damu yake Yesu.

Wema wala amani,

Bila damu yake Yesu.

 

5. Yashinda ulimwengu,

Hiyo damu yake Yesu.

Na kutufikisha juu,

Hiyo damu yake Yesu.

 

6. Twaimba: Utukufu

Una damu yake Yesu.

Milele twaisifu,

Hiyo damu yake Yesu.

 

79 Msalaba wa aibu

 

1. Msalaba wa aibu,

Ulinipa amani;

Uliniondoa kifungoni,

Nilimotesekea.

 

2. Ee, Mwokozi wangu, Yesu

Nitamwendea nani?

Najiweka msalabani,

Nikaoshwe damuni.

 

3. Nakupenda Bwana Yesu,

Kwa kunipenda kwako,

Napendezwa nikutumikie

Maisha yangu yote.

 

4. Usifiwe Bwana Yesu,

Kwa ulivyonifia,

Aleluya, nakushukuru,

Uliyenikomboa.

 

5. Msalaba ulishinda

Nguvu zake adui,

Ili mimi nikombolewe,

Niwe mwana wa Mungu.

 

80 Wamwendea Yesu kwa kusafiwa

 

1. Wamwendea Yesu kwa kusafiwa,

Na kuoshwa kwa damu ya kondoo?

Je neema yake umemwagiwa,

Tumeoshwa kwa damu ya kondoo?

 

Kuoshwa, kwa damu,

Itutakasayo ya kondoo;

Ziwe safi nguo nyeupe mno;

Umeoshwa kwa damu ya kondoo?

 

2. Wamwandama daima mkombozi

Na kuoshwa na damu ya kondoo?

Yako kwa msulubiwa makazi,

Umeoshwa kwa damu ya kondoo?

 

3. Atakapokuja Bwana –arusi

Uwe safi kwa damu ya kondoo!

Yafae kwenda mbinguni mavazi

Yafuliwe kwa damu ya kondoo.

 

4. Yatupwe yaliyo na takataka,

Na uoshwe kwa damu ya kondoo.

Huoni kijito chatiririka

Na uoshwe kwa damu ya kondoo?

 

81 Chini ya msalaba

 

1. Chini ya msalaba

Nataka simama;

Ndio mwamba safarini,

Wa kivuli chema;

Ni kweli kwa roho yangu

Ni tuo kamili,

Tatua mzigo wangu

Wakati wa hari.

 

2. Hapa ni pema sana,

Ni ngome kamili;

Hapa yameonekana,

Mapenzi ya kweli;

Kama alivyoonyeshwa

Yakobo zamani,

Msalaba umekuwa

Ngazi ya Mbinguni.

 

3. Na Yesu msalabani

Walimkemea,

Alikufa niokoke

Niliyepotea;

Naona ajabu sana

Ya mambo mawili

Jinsi alivyonipenda,

Nisiyestahili.

 

4. Atakayeonana,

Na Yesu Mbinguni,

Njia yake aanzapo

Ni msalabani;

Wokovu upo hapa tu,

Mwingine hapana,

Kisha kuna furaha kuu

Pamoja na Bwana.

 

82 Sioni haya kwa Bwana

 

1. Sioni haya kwa Bwana

Kwake nitang’ara!

Mti wake sitakana,

Ni neno imara!

 

Msalaba ndio asili ya mema,

Nikatua mzigo hapo;

Nina uzima, furaha daima,

Njoni kafurahini papo.

 

2. Kama kiti chake vivyo

Ni yake ahadi,

Alivyowekewa navyo

Kamwe havirudi.

 

3. Bwana wangu, tena Mungu

Ndilo lake jina!

Hataacha roho yangu

Wala kunikana.

 

4. Atakiri langu jina,

Mbele za Babaye,

Anipe pahali tena

Mbinguni nikae.

 

83 Kwa wingi wa nyama

 

1. Kwa wingi wa nyama,

Na sadaka pia,

Hupata wapi salama,

Kwondoa hatia?

 

2. Sadaka ni Yesu,

Hwondoa makosa;

Dhabihu mwenye jina kuu,

Atanitakasa.

 

3. Kwa yangu imani,

Nikuweke sasa

Mkono mwako kichwani

Kukiri makosa.

 

4. Roho yakumbuka

Mambo ya mtini,

Mzigo ulijitweka,

Ndiyo yangu deni.

 

5. Deni hutanguka,

Tukimuamini;

Kwa damu tumeokoka,

Twimbe furahani.

 

84 Niwonapo mti bora

 

1. Niwonapo mti bora

Kristo aliponifia

Kwangu pato ni hasara

Kiburi nakichukia.

 

2. Na nisijivune, Bwana

Ila kwa mauti yako;

Upuzi sitaki tena,

Ni chini ya damu yako.

 

3. Tangu kichwa hata nyayo,

Zamwagwa pendo na hamu,

Ndako pweke hamu hiyo,

Pendo zako zimetimia.

 

4. Vitu vyote vya dunia,

Si sadaka ya kutosha;

Pendo zako zinawia

Nafsi, mali, na maisha.

 

85 Ni mtu wa simanzi

 

1. Ni “Mtu wa Simanzi”,

Mwana wa mwenye enzi

Mwenye mengi mapenzi!

Asifiwe Bwana Yesu!

 

2. Akawa matesoni,

“Mungu mwana yakini

Akatoka Mbinguni:

Asifiwe Bwana Yesu!

 

3. Akapata dhihaka,

Mzoea – mashaka

Ndiye yetu sadaka:

Asifiwe Bwana Yesu!

 

4. Tu wenye dhambi sana;

Kwake dhambi hamna,

Na Mungu twapatana:

Asifiwe Bwana Yesu!

 

5. Alikufa mtini,

Akalia dhikini,

Sasa yuko Mbinguni:

Asifiwe Bwana Yesu!

 

6. Punde atarejea,

Yesu kutunyakua,

Ndipo tutamwimbia:

Asifiwe Bwana Yesu!

 

86 Damu imebubujika

 

1. Damu imebubujika,

Ni ya Imanweli,

Wakioga wenye taka,

Husafiwa kweli.

 

2. Ilimpa kushukuru

Mwivi mautini;

Nami nisiye udhuru,

Yanisafi ndani.

 

3. Kondoo wa kuuawa,

Damu ina nguvu,

Wako wote kuokoa,

Kwa utimilivu.

 

4. Bwana tangu damu yako

Kunisafi kale,

Nimeimba sifa zako;

Taimba milele.

 

5. Nikifa tazidi kwimba

Sifa za wokovu

Ulimi ujaponyamaa

Vumbini mwa ufu.

 

6. Bwana, umenikirimu

Nisiyestahili

Kwa damu yako, sehemu

Ya mali ya kweli.

 

7. Nikubali kukwimbia,

Mbinguni milele,

Mungu nitakusifia

Jina lako pweke.

 

87 Deni ya dhambi ilimalizika

 

1. Deni yangu ya dhambi,

Yesu amelipa.

Kwake msalabani

Nilipewa uzima.

 

Deni ya dhambi,

Msalabani,

Ilimalizikia,

Ni huru kabisa.

 

2. Bwana Yesu asema,

“Mwanangu dhaifu,

Uwezo wa ushindi

Hupatikana kwangu.”

 

3. Bwana, kweli naona,

Nguvu zako pekee

Huondoa ukoma,

Niwe kipya kiumbe.

 

4. Sina wema moyoni,

Nidai neema,

Nakubali kabisa,

Kwa damu kusafiwa.

 

5. Hata huko Mbinguni

Miguuni pake,

“Yesu alinifia,”

Nitaimba milele.

 

88 Ndiyo damu ya Baraka

 

1. Ndiyo damu ya baraka ituoshayo wakosa,

Kwake Bwana twaokoka, nasi twamsifu sasa;

Nimestahili hukumu, siwezi kujitakasa;

Nioshe katika damu, takuwa safi kabisa.

 

Safi kabisa; safi kabisa!

Nioshe katika damu;

Takuwa safi kabisa.

 

2. Yesu alivikwa miiba, na kuangikwa Mtini,

Na maumivu si haba yaliyompata chini.

Nataka kijito hicho niende kuoga sasa;

Ndicho kinitakasacho, nami ni safi kabisa.

 

Safi kabisa; safi kabisa!

Ndicho kinitakasacho,

Nami ni safi kabisa.

 

3. Baba, kweli nimekosa, moyo wangu ni dhaifu;

Dhambi ni nyingi kabisa, nipate wapi wokovu?

Yesu kijitoni pako, naja naamini sasa;

Nioshe kwa damu yako, takuwa safi kabisa.

 

Safi kabisa; safi kabisa!

Nioshe kwa damu yako,

Nami ni safi kabisa.

 

89 Kwa Kalvari

 

1. Muda mwingi nilipotea,

Sikufahamu msalaba,

Wala aliyenifilia,

Kwa Kalvari.

 

Rehema bure na neema,

Samaha nalo nilipewa,

Ndipo aliponifungua

Kwa Kalvari.

 

2. Kwa neno lake Bwana Mungu,

Nilijiona mimi mwovu,

Nikageuka na kutubu,

Kwa Kalvari.

 

3. Yote kwa Yesu namtolea,

Ndiye mfalme wa pekee sasa,

Kwa furaha nitamwimbia,

Wa Kalvari.

 

4. Jinsi pendo lilivyo kuu,

Neema ilishuswa toka juu,

Alitufanyia wokovu

Kwa Kalvari.

 

90 Aliteswa, aliteswa

 

1. Aliteswa, aliteswa,

Msalabani Yesu aliteswa,

Dhambi zangu ameziondoa,

Mahali pangu aliumizwa.

 

2. Alikufa, alikufa,

Msalabani Yesu alikufa,

Kwa kifo chake nakombolewa,

Kwa kuwa Yesu alinifia.

 

3. ’Kafufuka, ‘kafufuka,

Kaburini Yesu alitoka,

Nami nimewekwa huru pia,

kwa kuwa Yesu alifufuka.

 

4. Yuko hai, yuko hai,

Mbinguni anaishi Mwombezi,

Daima huniombea mimi,

Kwa kuwa Yesu adumu hai.

 

5. Atarudi, atarudi,

Siku moja Yesu atarudi,

Na tutamwonapo tutafurahi,

Kwa kupelekwa kwake Mbinguni.

 

6. Sifa kwake, sifa kwake,

Mbinguni na huimbwa milele,

Kwa furaha, masifu, na shangwe,

Tutamwimbia Yesu milele.

 

91 Mapenzi yako yafanyike, Bwana

 

1. Mapenzi yako yafanyike,

Wewe mfinyanzi, nami towe,

Unifinyange upendavyo,

Mimi tayari, naja kwako.

 

2. Mapenzi yako yafanyike,

Unihoji dhambi zote,

Unisafishe vya kimwili,

Niinamapo Msalabani.

 

3. Mapenzi yako yafanyike,

Mimi dhaifu, mimi mnyonge.

Uwezo wote, kwako kweli,

Sasa niponye, Ee, Mwokozi.

 

4. Mapenzi yako yafanyike,

Natoa kwako vitu vyote,

Maisha, mali, moyo, mwili,

Vyote ni vyako, kweli, kweli.

 

5. Mapenzi yako yafanyike,

Mapenzi yangu yavunjike,

Ninakubali uwe Bwana,

Ni mali yako, twaa kabisa.

 

6. Mapenzi yako yafanyike,

Unitawale siku zote,

Sura ya Yesu umba kwangu,

Nijaze Roho nayo nguvu.

 

92 Nataka nimjue Yesu

 

1. Nataka nimjue Yesu,

Na nizidi kumfahamu,

Nijue pendo lake, na

Wokovu wake kamili.

 

Zaidi, zaidi, nimfahamu Yesu,

Nijue pendo lake, na

wokovu wake kamili.

 

2. Nataka nione Yesu,

Na nizidi kusikia,

Anenapo kitabuni,

Kujidhihirisha kwangu.

 

3. Nataka nifahamu, na

Nizidi kupambanua

Mapenzi yake, nifanye

Yale yanayompendeza.

 

4. Nataka nikae naye,

Kwa mazungumzo zaidi,

Nizidi kuwaonyesha

Wengine wokovu wake.

 

93 Bwana amefufuka

 

1. Bwana amefufuka, Aleluya.

Twimbe na malaika, Aleluya.

Sifa zetu na shangwe, Aleluya.

Na zao zisitengwe, Aleluya.

 

2. Ukombozi timamu, Aleluya.

Umetimu kwa damu, Aleluya.

Mshindi asifiwe, Aleluya.

Yu hai kwa milele. Aleluya.

 

3. Jiwe, lindo, muhuri, Aleluya.

Vi wapi? Na kaburi? Aleluya.

Kifo hakimuweki, Aleluya.

Ametoka peponi, Aleluya.

 

4. Yu hai mtukufu; Aleluya.

Cha kifo hatuhofu! Aleluya.

Alitufia sisi, Aleluya.

Tuwe mahuru nasi, Aleluya.

 

5. Kichwa chatangulia, Aleluya.

Tupae, nasi, pia!, Aleluya.

Kwa kuwa tuna fungu, Aleluya.

Mti, kaburi, mbinguni, Aleluya.

 

6. Ndiwe Mwokozi wetu, Aleluya.

Sifa ni yako Yesu, Aleluya.

Utukuzwe pekeo, Aleluya.

Ni wewe ufufuo, Aleluya.

 

94 Siku ya mbingu kujawa na sifa

 

1. Siku ya Mbinguni kujawa na sifa,

Dhambi zilizidi duniani;

Yesu akaja azaliwe mtu,

Awe na watu ulimwenguni.

 

Alinipenda, alinifia,

Ameondoa na dhambi zangu;

Alifufuka nipewe haki,

Yuaja tena Mwokozi wangu.

 

2. Na siku moja walikwenda naye,

Wakamkaza msalabani;

Aliumia, aliaibishwa,

Ili atuokoe dhambini.

 

3. Siku hiyo wakamlaza chini

Kaburini alipumzika;

Matumaini yetu wenye dhambi,

Ni mwokozi, kwake twaokoka.

 

4. Kaburi likashindwa kumshika;

Jiwe likatoka mlangoni,

Alifufuka kwa kushinda kwake,

Naye yuko milele Mbinguni.

 

5. Siku moja atatujia tena;

Utukufu wake tutaona;

Atawaleta na wapenzi wetu;

Mwokozi: wangu, tutaonana.

 

95 Hivi vita vimekoma

 

Aleluya! Aleluya! Aleluya!

 

1. Hivi vita vimekoma,

Vimeshindwa na uzima,

Na asifiwe daima,

Bwana Yesu.

 

2. Nguvu za kifo ni hizo,

Ila hazina uwezo,

Ndizo sasa avunjazo,

Bwana Yesu.

 

3. Siku tatu za huzuni,

Kisha atoka ufuni,

Asifiwe duniani,

Bwana Yesu.

 

4. Mapingu ameyavunja,

Mbingu amezifungua,

Nasi sasa twamwimbia,

Bwana Yesu.

 

5. Na ulivyopigwa wewe,

Ni kwamba tufunguliwe,

Milele na usifiwe,

Bwana Yesu.

 

96 Mle kaburini, Yesu mwokozi

 

1. Mle kaburini, Yesu Mwokozi!

Alilazwa chini, Bwana wangu!

 

Bwana! Amefufuka,

Kifo kimeshindwa kabisa!

Gizani mle alitoka chini,

Sasa atawala huko Mbinguni!

Yu hai! Yu hai!

Bwana Yesu yu hai!

 

2. Aungoja huo, Yesu Mwokozi!

Mchana ujao, Bwana wangu!

 

3. Walinda kaburi, Yesu Mwokozi!

Bure ni muhuri, Bwana wangu!

 

4. Kifo kimeshindwa, Yesu mwokozi!

Pingu zimevunjwa, Bwana wangu!

 

 

97 Tazameni huyo ndiye

 

1. Tazameni huyo ndiye,

Mwenye kushinda vita;

Haya, tumsujudie;

Nyara anazileta;

Watu wote msifuni,

Sasa yumo kitini.

 

2. Msifuni malaika,

Mtukuzeni sana,

Wote waliookoka

Watamsifu Bwana;

Watu wote msifuni,

Sasa yumo kitini.

 

3. Walimfanya dhihaka

Zamani wenye shari,

Kwao waliookoka

Ni Bwana wa fahari;

Watu wote msifuni.

Sasa yumo Kitini.

 

4. Nyimbo nzuri, sikizeni,

Ni nyimbo za sifa kuu,

Za Bwana Yesu kitini,

Kutawazwa, yeye tu;

Watu wote msifuni

Sasa yumo Kitini.

 

98 Huyo ndiye anashuka

 

1. Huyo ndiye! anaskuka,

Aliyetufilia,

Wengi waliookoka,

Wakimfurahia,

Aleluya!

Yesu aturudia.

 

2. Sote tutamtazama,

Amekaa kitini,

Nao waliomcoma,

Kumkaza mtini,

Na kilio, wamuone enzini.

 

3. Alama za kifo chake

Hata sasa anazo

Na waaminifu wake

Wapendezewa nazo.

Alipata,

Kwetu alama hizo.

 

4. Wokovu utakiwao

Sasa wapatikana,

Na watakatifu hao

Mbinguni wakutana

Kumlaki,

Ndiyo siku ya Bwana

 

5. Wakusujudie wote

Mbele ya kiti chako.

Zako, Bwana, nguvu zote

Itwae milki yako

Njoo Bwana,

Sisi tu watu wako.

 

99 Maelfu na maelfu

 

1. Maelfu na maelfu

Wenye nguo bora!

Masafu ya waongofu

Wenye na bendera!

Amekwisha kamili

Vita vya shetani

Fungueni lango hili;

Njoni, ingieni!

 

2. Imbeni aleluya,

Zipae Mbinguni!

Pigeni sana sauti

Kwa kutumaini!

Kwa hiyo viliumbwa

Nchi hata Mbingu

Dhiki za muda zikisha,

Asifiwe Yesu.

 

3. Loo! Tukionana

Pwani ya ng’amboni!

Loo! Tukishirikiana

Milele Mbinguni!

Midomo yote pia,

Huko itaimba

Wajane kufufukiwa

Na kila yatima!

 

4. Himiza enzi yako,

Uliyetufia

Utimize watu wako,

Wakosaji pia,

Mpendwa wa taifa

twakutumaini!

Uzifunue ishara

Urudi enzini!

 

100 Tumrudie Bwana

 

1. Mbona washangaa njiani?

Mbona warejea nyuma?

Warudi tena gizani

Alimokutoa Bwana?

 

2. Ni ya bure yote haya,

Uliyofunzwa ya Mungu?

Ni bure amekufia

Bwana Yesu kwa uchungu?

 

3. Wamtia kristo aibu

Na maneno yake pia?

Siku yaja ya hesabu,

Utamjibuje Bwana?

 

4. Upandapo tena hayo,

Halafu utayavuna.

Rudi kwa Bwana upesi,

Mwombe akupokee tena.

 

101 Twonane milele

 

1. Nyimbo na tuziimbe tena

Za alivyotupenda mbele;

Kwa damu ya thamani sana!

Mbinguni twonane milele.

 

Twonane milele,

Twonane bandarini kule;

Twonane milele,

Twonane bandarini kule.

 

2. Hupozwa kila aoshwaye,

Kwa damu ya Kondoo yule;

Ataishi afurahiye

Vya Yesu mbinguni milele.

 

3. Hata sasa hufurahia

Tamu yake mapenzi yale,

Je, kwake tukifikilia,

Kutofarakana milele?

 

4. Twende mbele kwa jina lake,

Hata aje mwokozi yule,

Atatukaribisha kwake,

Tutawale naye milele.

 

5. Sauti zetu tuinue

Kumsifu Mwokozi yule,

Ili watu wote wajue

Wokovu u kwake milele.

 

102 Kazi yangu ikiisha

 

1. Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka;

Na kuvaa kutokuharibika,

Nitamjua Mwokozi nifikapo ng’amboni;

Atakuwa wa kwanza kunilaki.

 

Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso;

Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari.

 

2. Furaha nitapata nikiona makao

Bwana aliyotuandalia;

Nitamsifu mwokozi kwa rehema na pendo

Vilivyonipa pahali Mbinguni.

 

3. Nao waliokufa katika Bwana Yesu,

Nitawaona tena huko juu;

Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni,

Nataka kumwona Mwokozi kwanza.

 

4. Milangoni mwa mji Bwana atanipitisha,

Pasipo machozi wala huzuni.

Nitauimba wimbo wa milele; lakini

Nataka kumwona Mwokozi kwanza.

 

103 Kaa nami

 

1. Kaa nami, ni usiku tena;

Usiniache gizani, Bwana;

Msaada wako haukomi;

Nili peke yangu, kaa nami.

 

2. Siku zetu hazikawi kwisha,

Sioni la kunifurahisha;

Hakuna ambacho hakikomi,

Usiye na mwisho kaa nami.

 

3. Nina haja nawe kila saa;

Sina mwingine wa kunifaa;

Mimi nitaongozwa na nani

Ila wewe? Bwana, kaa name.

 

4. Sichi neno uwapo karibu;

Nipatalo lote, si taabu;

Kifo na kaburi haviumi;

Nitashinda kwako, kaa nami.

 

5. Nilalapo nikuone wewe,

Gizani mote nimulikiwe;

Nuru za mbinguni hazikomi,

Siku zangu zote kaa nami.

 

104 Twasoma ni njema sana

 

1. Twasoma, ni njema sana

Mbinguni, kwa Bwana;

Twasoma, dhambi hapana,

Mbinguni kwa Bwana;

Malaika wema wako,

Vinanda vizuri viko,

Na majumba tele yako,

Mbinguni kwa Bwana.

 

2. Siku zote ni mchana,

Ni nchi ya raha;

Wala machozi hapana,

Ni nchi ya raha;

Walioko wanuona

Uso wa Mwokozi, tena

Jua jingine hapana,

Ni nchi ya raha.

 

3. Nyama na vitu viovu

Havimo kabisa;

Kifo nacho, na ubovu,

Havimo kabisa.

Ni watakatifu wote,

Wameoshwa dhambi zote;

Wasiosafiwa wote

Hawamo kabisa.

 

4. Tuna dhambi, pia sote,

Mwokozi akafa;

Kwake tutaoshwa zote,

Mwokozi akafa;

Kwake twapata wokovu,

Tutawona utukufu;

Mbinguni tutamsifu;

Mwokozi akafa.

 

5. Baba, mama, ndugu zetu,

Twendeni kwa Bwana;

Huku chini sio kwetu,

Twendeni kwa Bwana;

Tusishikwe na…

 

105 Kuwatafuta

 

1. Kuwatafuta wasioweza,

Kuomba wamrejee Yesu,

Kuwaambia maneno yake,

“Njooni kwangu, nawapenda”.

 

Nitakwenda, (kwenda), niwatafute

Waongofu (wa Bwana) wageuke,

Waingie (wote) katika zizi

La Mkombozi (wetu) Yesu kristo.

 

2. Kuwatafuta wasioweza,

Waonyeshwe Mwokozi wetu,

Kuwaongoza, wapate wote

Uzima wa milele.

 

3. Kazi hiyo nataka kufanya,

Leo nimesikia mwito

Kuwainua waangukao,

Waletwe kwake Yesu njia.

 

106 Mungu awe nanyi daima

 

1. Mungu awe nanyi daima,

Hata twonane ya pili,

Awachunge kwa fadhili,

Mungu awe nanyi daima.

 

Hata twonane huko juu,

Hata twonane kwake kwema;

Hata twonane huko juu,

Mungu awe nanyi daima.

 

2. Mungu awe nanyi daima;

Ziwafunike mbawaze,

Awalishe, awakuze;

Mungu awe nanyi daima.

 

3. Mungu awe nanyi daima;

Kila wakati wa shani

Awalinde hifadhini;

Mungu awe nanyi daima.

 

4. Mungu awe nanyi daima;

Awabarikie sana,

Awapasulie kina;

Mungu awe nanyi daima.

 

107 Ewe Baba wa Mbinguni

 

1. Ewe, Baba wa Mbinguni,

Usikie twombalo

Hapa chini duniani,

Na uwe radhi nalo

 

Ee Mungu, bariki

Ndugu hawa wawili!

Ee Mungu, bariki

Ndugu hawa wawili!

 

2. Watu hawa mbele zako,

Na mbele ya kanisa;

Watimize Neno lako

Wanakutana sasa.

 

3. Kama Yesu na Kanisa,

Ni mmoja, na hivyo,

Watu hawawape sasa

Wawe mmoja vivyo

 

4. Walinde, Bwana, daima,

Wabariki nyumbani

Uwape nyingi salama

Humu ulimwenguni.

 

5. Wabariki, ewe Bwana,

Watu hawa wawili,

Wape upaji wa wana,

Wafurahishwe kweli.

 

6. Siku za duniani

Zitakapopungua,

Wape kurithi Mbinguni

Mema ya kwendelea.

 

108 Twenenda sayuni

 

1. Mpendao Bwana

Ije raha yenu!

Imbeni nyimbo za raha

Wa ibada yenu.

 

Twenenda Sayuni,

Mji mzuri Sayuni;

Twenenda juu Sayuni

Ni maskani ya Mungu.

 

2. Wasiimbe wao

wasioamini,

Watoto wa Mungu ndio

waimbao chini.

 

3. Twaona rohoni

Baraka za Mungu,

Tusijafika Mbinguni

Kwenye utukufu.

 

4. Tutakapo mwona

Masumbuko basi,

Huwa maji ya uzima,

Anasa halisi.

 

5. Tupaaze sauti,

Na fute machozi,

Twenenda kwa Imanweli

Naye ni Mwokozi.

 

109 Nitaimba ya Yesu

 

1. Nitaimba ya Yesu,

Kwa rehema zake,

Baraka nyingi sana

Nimepata kwake;

Nitaimba ya Yesu,

Sadaka ya Mungu,

Alimwaga damu

Ukombozi wangu.

 

2. Nitaimba ya Yesu

Hapa siku zote,

Nitakapokumbuka

Vyema vyake vyote;

Nitaimba ya Yesu

Hata mashakani,

Yeye atanilinda

Mwake ubavuni.

 

3. Nitaimba ya Yesu

Niwapo Njiani;

Takaza Mwendo, hata

Nifike Mbinguni;

Nikiisha ingia

Mlangoni mle,

Yesu nitamwimbia

Mbinguni milele.

 

110 Mapya ni mapenzi hayo

 

1. Mapya ni mapenzi hayo,

Asubuhi tunayo,

Saa za giza hulindwa

Kwa uzima kuamshwa.

 

2. Kila siku, Mapya pia

Rehema, wema, na afya,

Wokofu, na msamaha,

Mawazo mema, furaha.

 

3. Tukijitahidi leo

Na mwendo utupasao,

Mungu atatueleza

Yatakayompendeza.

 

4. Mambo yetu ya dunia

Mungu atayang’aria,

Matata atageuza

Yawe kwetu ya Baraka.

 

5. Yaliyo madogo, haya

Mungu tukimfanyia,

Yatosha: tutafaidi

Huvuta kwake zaidi.

 

6. Ewe Bwana, siku zote,

Tusaidie kwa yote:

Mwendo wetu wote vivyo,

Uwe kama tuombavyo.

 

111 Neno lako Bwana

 

1. Neno lako, Bwana,

Ni imara sana;

Lilo latwongoza,

Lilo latufunza.

 

2. Adui wabaya

Wakikaribia,

Neno lake Bwana

Ni ulinzi sana.

 

3. Siku za dhoruba

Soma ukiomba;

Neno lake Bwana

Msaada sana.

 

4. Ukiliamini,

Hwenda na amani;

Una na furaha

Neno ni siraha.

 

5. Ni furaha kweli,

Na wingi wa mali,

Neno lake Bwana

Kwa wasiokana

 

6. Neno la rehema,

Tukali wazima;

Faraja I papo,

Tufarikanapo.

 

112 Nilikupa wewe maisha yangu

 

1. Nilikupa wewe

Damu ya moyoni,

Ili wokolewe,

Winuke ufuni:

Nimekunyimani?

Umenipa nini?

 

2. Nilikupa miaka

Yangu duniani

Upate inuka,

Kuishi Mbinguni:

Nimekunyimani?

Umenipa nini:

 

3. Niliacha nuru

Za Baba, Mbinguni,

Kwingia taabu

Za ulimwenguni:

Nimekunyimani?

Umenipa nini?

 

4. Niliteswa sana,

Mateso kifoni,

Usije yaona

Hayo ya motoni:

Nimekunyimani?

Umenipa nini?

 

5. Nimekuletea

Huku duniani

Upendo na afya

Zatoka Mbinguni:

Nimekunyimani?

Umenipa nini?

 

6. Nipe siku zako,

Udumu mwangani;

Na taabu yako,

Wingie rahani

Nafsi, pendo, mali,

Twae Imanweli.

 

113 Ni mfalme wa mapenzi

 

1. Ni Mfalme wa mapenzi

Ndiye anichungaye,

Sipungukiwi, hawezi.

Kunipoteza yeye.

 

2. Kando ya mji mazima

Yeye huniongoza

Katika malisho mema

Daima hunilaza.

 

3. Mara nyingi hupotea

Kwa ukaidi wangu,

Naye huniandamia,

Hunirudisha kwangu.

 

4. Uvulini mwa mauti,

Siachi hatari kamwe,

Wewe Bwana huniachi,

Mwokozi wangu wewe.

 

5. Waniandikia meza

Neema kwako tele.

Kwa wewe, yote naweza.

Na msalaba mbele.

 

6. Kamwe hautapungua

Uule wema wako;

Mwisho, atanichukua,

Juu, niimbe kwako.

 

114 Bwana Mungu, nashangaa kabisa

 

1. Bwana Mungu, nashangaa kabisa

Nikitazama kama vilivyo

Nyota, ngurumo, vitu vingi vyote

viumbwavyo kwa uwezo wako.

 

Roho yangu na ikuimbie

Jinsi Wewe ulivyo Mkuu,

Roho yangu na ikuimbie

Jinsi Wewe ulivyo Mkuu.

 

2. Nikitembea pote duniani,

Ndege huimba, nawasikia,

Milima hupendeza macho sana,

Upepo nao nafurahia.

 

3. Nikikumbuka kama Wewe Mungu

Ulivyompeleka Mwanao,

Afe azichukue dhambi zetu,

Kuyatambua ni vigumu mno.

 

4. Yesu Mwokozi utakaporudi

Kunichukua kwenda Mbinguni,

Nitashukuru na kwimba milele,

Wote wajue jinsi ulivyo.

 

115 Kilima kando ya Mji

 

1. Kilima kando ya mji

Alikufa Bwana;

Kuokoa wakosaji

Akateswa sana.

 

2. Kabisa hayasemeki,

Mateso dhaifu

Alikufa mwenye Haki

Tupate wokovu.

 

3. Alimwaga damu yake

Ili tuwe wema,

Tufae kukaa kwake

Mbinguni daima.

 

4. Hatuna mwenye imani

Aliye na haki,

Wa kutosha yetu deni,

Rafiki Yesu tu.

 

5. Alijua peke yake

Kufungu Mbingu

Ufunguo damu yake

Kondoo wa Mungu.

 

6. Aliyetupenda hivyo

Nasi tumpende,

Tukamtumai vivyo

Na kazi tutende.

116 Bwana , U sehemu yangu

 

1. Bwana u sehemu yangu,

Rafiki yangu wewe;

Katika safari yangu

Tatembea na wewe;

Pamoja na wewe,

Pamoja na wewe,

Katika safari yangu

Tatembea na wewe.

 

2. Mali hapa sikutaka,

Ili niheshimiwe,

Na yanikute mashaka

Sawa sawa na wewe,

Pamoja na wewe,

Pamoja na wewe,

Heri nikute mashaka

Sawasawa na wewe.

 

3. Niongoze safarini,

Mbele unichukue

Mlangoni kwa Mbinguni

Niingie na wewe.

Pamoja na wewe,

Pamoja na wewe,

Mlangoni kwa mbinguni,

Niingie na wewe.

 

117 Tufani inapovuma

 

1. Tufani inapovuma

Sana moyoni mwangu,

Huona pa kujificha

Mkononi mwa Mungu.

 

Hunificha, hunificha

Adui hatanipata,

Hunificha, hunificha,

Mkononi mwake.

 

2. Pengine kuna taabu

Yanisongeza kwake;

Naijua si hasira,

Ni ya mapenzi yake.

 

3. Adui wakiniudhi

Nami nikisumbuka,

Mungu atavigeuza

Vyote viwe baraka.

 

4. Niishipo duniani

Ni tufani daima,

Anilindapo rohoni

Nitakaa salama.

 

118 Ni ujumbe wa Bwana

 

1. Ni ujumbe wa Bwana, Aleluya!

wa maisha ya daima,

Amenena mwenyewe, Aleluya!

Utaishi ukitazama.

 

Tazama, ishi sasa!

Kumtazama Yesu,

Amenena mwenyewe, Aleluya!

Utaishi ukitazama.

 

2. Ni ujumbe wa wema, Aleluya!

Nawe shika, rafiki yangu!

Ni habari ya raha Aleluya!

Mwenye kuinena ni Mungu.

 

3. Uzima wa daima,Aleluya !

Kwake Yesu utauona.

ukimtazama tu, Aleluya!

Wokovu u pweke kwa Bwana.

119 Si damu ya nyama

 

1. Si damu ya nyama

Iliyomwagika

Iwezayo kuondoa

Dhambi za wakosa.

 

2. Yeye Bwana Yesu

Sadaka ya Mungu,

Mwenye damu ya thamani,

Ni mwokozi kweli.

 

3. Kwa imani yangu,

Namshika yeye,

Naziweka dhambi zangu

Juu ya kichwa chake.

 

4. Mzigo wa dhambi

Sichukui tena,

Ameuchukua yeye,

Juu ya msalaba.

 

5. Bwana Yesu ndiye,

Mwokozi wa kweli

Tumsifu siku zote,

Twapata uhuru.

 

120 Enyi wanadamu

 

1. Enyi wanadamu mbona

Sana mwatanga-tanga,

Kama kondoo wanyonge,

Wasio na mchunga?

Yuko mchunga mmoja

Mwenye mapenzi mema;

Haya kutaneni kwake,

Atawachunga vyema.

 

2. Mungu tunamwona kuwa

Mwenye uwezo wote;

Na nguvu zake zapita

Mawazo yetu yote:

Ni Baba,mapenzi yake

Ni makubwa hakika;

Hatuwezi kuyajua,

Na hayana mpaka.

 

3. Rehema za Mungu nazo

Zina upana sana;

Kama huo wa bahari,

Mwisho wake hapana;

Haki yake ina mema,

Kwa hayo twashukuru,

Kwetu uko msamaha,

Furaha na uhuru.

 

4. Mapenzi yake mapana,

Sisi hatuna cheo

Cha kutosha, nao moyo

Una wema upeo;

Ukombozi mwingi mno

Katika damu yake;

Sote twapata furaha,

Kwa maumivu yake.

 

5. Yesu mkaribieni

Njoni msife myoyo;

Njoni kwake kwa imani,

Mema yake ni hayo;

Heri tuwe kama wana

Tush…

121 Liko lango moja wazi

 

1. Liko lango moja wazi,

Ni lango la mbinguni;

Na wote waingiao

Watapata nafasi.

 

Lango ndiye Yesu Bwana

Wote waingie kwake,

Lango! Lango

La Mbinguni ni wazi.

 

2. Yesu ndiye lango hili,

Hata sasa ni wazi,

Kwa wakubwa na wadogo,

Tajiri na maskini.

 

3. Hili ni lango la raha,

Ni lango la rehema;

Kila mtu apitaye

Hana majonzi tena.

 

4. Tukipita lango hili

Tutatua mizigo,

Tuliochukua kwanza,

Tutavikwa uzima.

 

5. Hima ndugu tuingie

Lango halijafungwa,

Likifungwa mara moja

Halitafunguliwa.

 

122 Bwana Yesu

 

1. Bwana Yesu, Bwana Yesu,

Mbona unaumia? Unateseka sana,

Kwa ajili ya kuomba,

Waomba na jasho jingi likageuka damu.

 

Kumbe! Ni dhambi zangu zinazokuumiza.

Bwana wangu, Mungu wangu,

Mimi leo, naja kwako

Ili niziungame.

 

2. Bwana Yesu, Bwana Yesu,

Mbona unaumia, na mizigo mizito?

Umejitwalia wewe, msalaba mabegani

Kwa ajili ya watu.

 

3. Bwana Yesu, Bwana Yesu,

Mbona unatukanwa, wawambwa kama mwizi,

Bila kosa ukalia, Baba yangu, wasamehe,

Chukua roho yangu.

 

4. Bwana Yesu, Bwana Yesu,

Muda ulipofika, nchi ikawa giza,

Mbinguni pakatulia,

Angani pakawa kimya,

Watu wakaogopa.

 

5. Bwana Yesu, Bwana Yesu,

Jinsi ulivyoumwa, ukamwomba Baba,

Leo umeshinda kifo, sasa wapaa Mbinguni,

Naimba, Haleluya.

 

123 Nimeketi mimi nili kipofu

 

1. Nimeketi mimi nili kipofu

Gizani nangojea macho;

Ewe Bwana Yesu mwenye wokovu,

Ondoa dhambi zangu nzito.

 

Huruma hakuna aonaye,

Gizani nagojea macho,

Sasa nitakase nikusihiye,

Yesu, na dhambi zangu nzito.

 

2. Tangu siku nyingi nimepofuka

Natamani uso nikwone;

Ewe Bwana Yesu, mwenye baraka

Sema neno, basi, nipone.

 

3. Nimeketi mimi nili na giza,

Nami ya kutumai sina;

Ili nasikia kunong’oneza,

“Kwake Yesu kuna kupona.”

 

124 Mungu ulisema

 

1. Mungu ulisema,

Giza ilikoma;

Twakushukuru!

Twakusihi sote,

Duniani mote

Na kwa watu wote,

Iwe nuru.

 

2. Yesu ulikuja,

Ulituletea

Nuru kuu;

Macho kwa vipofu,

Maisha kwa wafu;

Twakushukuru.

 

3. Roho kiongozi,

Roho wa mapenzi

Tia nuru;

Mwovu hata sasa

Watu huwatosa,

Tunakwomba hasa,

Iwe nuru.

 

4. Mungu wa utatu

Mwanga wao watu,

Tuwe huru;

Twende kote-kote

Wafundishwe wote,

Duniani mote,

Iwe nuru.

 

125 Ati twonane Mtoni?

 

1. Ati twonane mtoni?

Maji mazuri ya Mbingu;

Yanatokea mwangani,

Penye kiti cha Mungu.

 

Naam, twonane mtoni!

Watakatifu, kwenu ni mtoni!

Tutakutanika mtoni

Penye kiti cha Mungu.

 

2. Tukitembea mtoni

Na Yesu mchunga wetu

Daima tu ibadani

Usoni pake kwetu.

 

3. Kwang’ara sana mtoni

Cha Mwokozi ni kioo,

Milele hatuachani,

Tumsifu kwa nyimbo.

 

4. Si mbali sana mtoni,

Karibu tutawasili,

Mara huwa furahani

Na amani ya kweli.

 



 

1. Ni mji mzuri,

Mbali sana;

Watu wanawiri

Kama jua;

Waimba kwa tamu,

Tuna wema hakimu:

Sifa na idumu,

Kwake Bwana.

 

2. Ni mji mzuri

Twende sote!

Una na fahari

Msikawe!

Raha tutaona,

Dhambi hapana tena;

Hatutaachana

Siku zote.

 

3. Ni mji mzuri;

Macho yote

Huko wanawiri

Kama pete;

Baba tutamwona,

Tukifanywa tu wana;

Tumo kupendana

Naye sote.

 

4. Ni mji mzuri;

Tusipotee

Na tuwe hodari,

Tuupate!

Tufunze, tutume

Kwa taji na ufalme:

Sifa na zivume

Siku zote.

 

127 Bwana Yesu atakuja

 

1. Bwana Yesu atakuja, Vumilia!

Omba, ukiwa na haja, Vumilia!

Mbingunu Mungu aliko, Mwamini Mwokozi wako,

Nawe utafika huko, Vumilia!

 

2. Ikikucheka dunia, Vumilia!

Mwovu atakuvizia, Vumilia!

Hataweza kukushinda, Bwana Yesu akulinda,

Roho yako, akupenda, Vumilia!

 

3. Na ukiwa hatarini, Vumilia!

Dhiki nyingi duniani, Vumilia!

Vyatupasa kuyakuta, Majaribu na matata,

Na Bwana hakutuficha; Vumilia!

 

4. Adui wakikutana, Vumilia!

Na ndugu wakikukana, Vumilia!

Zote, zote zitakwisha, Nguvu zote za kutisha

Mungu chini atashusha; Vumilia!

 

5. Moyoni una majonzi, Vumilia!

Ndiyo bonde-ya-machozi, Vumilia!

Hima tutaandamana, Kwetu Mbinguni na Bwana

Tena hatutaachana; Vumilia!

 

128 Mmoja apita wote

 

1. Mmoja apita wote,

Atupenda;

Zaidi ya ndugu wote,

Atupenda;

Rafiki wa duniani,

Wote hatuwaamini;

Yesu kwa kila zamani,

Atupenda.

 

2. Kumjua ni uzima,

Atupenda;

Jinsi ajaavyo wema

Atupenda;

Yeye ametununua

Kwa damu aliyomwaga,

Dhambini kutuokoa,

Atupenda.

 

3. Sasa tunaye rafiki,

Atupenda;

Hupenda kutubariki;

Atupenda;

Twapenda kumsikia,

Atwita kukaribia,

Nasi tutamwamania,

Atupenda.

 

4. Husamehe Dhambi zetu,

Atupenda;

Hushinda adui zetu,

Atupenda;

Anatwonea huruma,

Hatupati ila mema,

Anatwongoza salama,

Atupenda.

 

129 Karibu na wewe

 

1. Karibu na wewe,

Mungu wangu

Karibu zaidi,

Bwana wangu

Siku zote niwe

Karibu na wewe,

Karibu zaidi

Mungu wangu.

 

2. Mimi nasafiri

Duniani,

Pa kupumzika

Sipaoni,

Nilalapo niwe

Karibu na wewe,

Karibu zaidi

Mungu wangu.

 

3. Na kwa nguvu zangu

Nikusifu;

Mwamba, uwe maji

Ya wokovu;

Mashakani niwe

Karibu na wewe;

Karibu zaidi

Mungu wangu.

 

4. Na nyumbani mwa juu,

Baba yangu,

Zikikoma hapa

Siku zangu,

Kwa furaha niwe

Pamoja na wewe,

Karibu kabisa

Mungu wangu.

 

130 Niongoze, Bwana Mungu

 

1. Niongoze, Bwana Mungu,

Ni msafiri chini;

Ni mnyonge, nguvu sina:

Nishike mkononi;

U mkate wa Mbinguni,

nilishe siku zote.

 

2. Kijito cha maji mema,

Kitokacho mwambani,

Nguzo yako, moto, wingu,

Yaongoza jangwani;

Niokoe mwenye nguvu;

Nguvu zangu na ngao.

 

3. Nikikaribia kufa,

Sichi neno lolote,

Wewe kifo umeshinda

Zinawe nguvu zote,

Tutaimba sifa zako,

Kwako juu milele.

 

131 Piga sana vita vyema

 

1. Piga sana vita vyema

Kwa ushujaa daima,

Yesu ndiye nguvu zako,

Yesu ndiye kweli yako.

 

2. Kaza mwendo, ushindane

Angaza macho, umwone

Yesu ndiye njia yako,

Naye ndiye tuzo lako.

 

3. Tupa kizito, simama,

Tazama mbele, si nyuma;

Ni yeye uzima wako,

Naye ni kipendo chako.

 

4. Tangamka, uamini

Akushika mikononi

Hageuki, akupenda,

Kuwa naye una pia.

 

132 Sauti sikilizeni

 

1. Sauti sikilizeni

Za waimbao juu,

“Aleluya, Aleluya,

Aleluya, mkuu!”

Wako makundi-makundi

Kama nyota wang’ara,

Kwa makuti ya mitende,

Na meupe wamevaa.

 

2. Wazazi na manabii

Wafanyaji wa njia;

Mashahidi, waandishi,

Nao wafalme pia!

Mabikira kina-mama,

Wajane wa kusali,

Waimba wakikutana

“Msifunu Imanweli”.

 

3. Watu toka huzunini

Wameosha na nguo,

Ni kwa damu yake Yesu;

Maonjo, mbali nao!

Walitekwa, walikatwa

Hata kwa misumeno,

Kwao kifo na shetani

Walishindiwa mno.

 

4. Mungu mumo mwake Mungu,

Nuru mumu mwa nuru,

Kwa kufungamana mwako

Tutaishi mahuru;

Tujalize, Imanweli,

Kujaa kwako wewe

Mungu Baba, Mungu Mwana,

Mungu Roho, tunawe.

 

133 Ni wako Mungu

 

1. Ni wako Mungu!

Ni furaha kwangu,

Ni raha kumjua mwokozi wangu.

 

Aleluya enzi ndako;

Aleluya,Amin.

Aleluya,enzi ndako;

Rejea Yesu.

 

2. Mwana wa Mungu

Ndiye fungu langu,

Na moyo hufurahi kwa Yesu wangu.

 

3. Raha ya kweli

Ina jina hili,

Na aliyeshika,ana Mbingu kweli.

 

4. Nimeingia

Mapendano haya,

Nimepata uzima na Mbingu pia.

 

5. Nilipo chini,

Ni mwako kazini

Hata nije kwako uliko Mbinguni.

134 Juu yake langu shaka

 

1. Juu yake langu shaka,

Yesu namuwekea,

Nami sitafedheheka

Nikimtegemea.

 

Natumai, natumai,

Nnatumai kwake tu;

Natumai, natumai,

Natumai kwake tu.

 

2. Juu yake, dhambi zangu;

Aniosha kwa damu;

Nionekane kwa Mungu,

Nisiye na laumu.

 

3. Juu yake yangu hofu;

Kwake nimetulia;

Sipotei kwa upofu

Njia aning’azia.

 

4. Juu yake raha yangu;

Humuangalia tu;

Mwenye kila ulimwengu,

Aniruzuku na huu.

 

5. Juu yake, moyo wangu;

Hali yangu na mali;

Mimi wake, Yeye wangu,

Twapasana kamili.

 

135 Mapenzi ya milele

 

1. Mapenzi ya milele

Ndiyo yanipendezayo;

Yalinipenda mbele,

Sina fahamu nayo;

Sasa amani yake

Tele rohoni mwangu,

Ni mimi kwa kuwa wake,

Na yeye kuwa wangu,

Ni mimi kuwa wake,

Na yeye kuwa wangu

 

2. Mbingu zinang’ara juu,

Na nchi nayo vivyo;

Macho ya dunia tu

Hayajaona hivyo;

Nyuni huimba sana,

Maua yana rangi,

Ni kumjua Bwana

Na pendo zake nyingi,

Ni kumjua Bwana

Na pendo zake nyingi,

 

3. Mambo mengi maovu

Nayo yenye kutisha,

Sasa hayana nguvu,

Si yenye kututisha;

Ni mkononi mwake,

Nalindwa salamani

Ninajua ni wake,

Ni wake mapenzini.

Ninajua ni wake,

Ni wake mapenzini.

 

4. Wake hata milele,

Si kutengana tena;

Hunipa raha tele

Moyoni mwangu, Bwana;

Hiyo nchi na Mbingu

Zitatoweka zile,

Ni wake, Yeye wangu,

Milele na milele.

Ni wak…

136 Msifuni, Yesu ndiye mkombozi

 

1. Msifuni ,Yesu ndiye mkombozi;

Imbeni ya pendo zake kuu,

Sujuduni,malaika mlioko,

Jina lake liwe na sifa kuu.

Kama vile mchunga uchungavyo

Vivyo sisi kutwa atachunga.

Msifuni mlio wakw watoto

Msifuni aliye mchunga.

 

2. Msifuni,Yesu ndiye mkombozi;

Akateswa tupate ongoka;

Ndiye Mwamba,Dhamana ya kuokoka;

Sujuduni kwake muangikwa,

Yesu aliyeudhiwa na hamu

Kwa pendo za baba yake Mungu.

Aliyefyolewa na kusulubiwa.

Msifuni ndilo letu fungu.

 

3. Msifuni,Yesu ndiye Mkombozi;

Shindukeni,enyi malango juu;

Bwana Yesu tangu milele Mwokozi,

Mvikeni taji, ni yake tu.

Atakuja kuitawala nchi,

Yesu,Mwombezi wetu wa Mungu.

Msifuni, ni mfalme wa salama;

Ndiye kweli mwana wake Mungu.

 

137 Yesu mponya

 

1. Yesu ndiye mganga wetu

Aponya wagonjwa wote;

Mganga wetu ni Yesu,

Aponyaye hasira.

 

Tumsifu huyo Yesu

Tumsifu milele,

Kwani Mponya mtakata

Mwokozi wa wanyonge

 

2. Mganga wetu ni Yesu

Huondoa matusi;

Mganga wetu ni Yesu,

Mwenye kuponya choyo.

 

3. Mganga wetu ni Yesu

Huponya wivu wetu;

Yesu ndiye aponyae

Kelele za nyumbani.

 

4. Mganga wetu ni Yesu

Mponya wa tamaa mbaya;

Mganga wetu ni Yesu

Uasherati hufuta

 

5. Mganga wetu ni Yesu

Aponya kiu cha pombe,

Mganga wetu ni Yesu

Kila dhambi uponya

 

138 Tukutendereza Yesu (Luganda)

 

1. Yesu, Mulokozi wange:

Lero nze wuwo wenka;

Omusaigwo gunazi’za

Yesu Mwana gwendiga.

 

Tukutendereza, Yesu,

Yesu Mwana gwendiga;

Omusaigwo gunazi’za;

Nkwebaza, Mulokozi.

 

 

2. Eda nafuba bufubi

Okufuna, emirembe;

Lero maliride dala

Okweyabiza Yesu.

 

3. Nababuliranga bantu

Obulokozi bwona,

Obutali bwa kitundu

Obulamba obwobuwa

 

4. Nategezanga ebya Yesu

Nobuvumunesitya;

Eyanziya mu busibe

Nokuwonya eyamponya.

 

5. Nebaza eyanunula nze;

Eyamponya wa kisa!

Yesu ankuma

Ansanyusaera,

Bulijo yebazibwe.

139 Nuru ya rohoni

 

1. Nuru ya rohoni

ni Bwana Yesu.

Nakuomba sana

niangazishe;

ukanitazame

kwa huruma tu,

 

/: ukanitulize

mimi maskini. :/

 

2. Futa dhambi zangu

kwa damu yako.

Hasira ya Mungu

iniondoke.

Machubuko yako,

hata mateso,

 

/: niyawaze vema

rohoni mwangu. :/

 

3. Nakutumaini

peke yako tu,

niwe mtumwa wako

pote nilipo

utanikubali

sina mashaka!

 

/: Nitakushukuru

pasipo mwisho. :/

 

 

140 Mahali ni pazuri

 

1. Mahali ni pazuri,

ndugu wanapokaa,

/: wakipatana vema,

na wakipendana. :/

 

2. Kama umande mzuri,

unyweshavyo shamba,

/: vivyo na Mungu wetu,

hubariki ndugu. :/

 

3. Upendano hujenga,

boma zuri kwao,

/: wakae na amani,

waliookakoka. :/

 

4. Na ulimwengu wote,

watiwa nuruni,

/: halafu kundi moja,

na mchunga mmoja tu. :/

 

 

141 Pana jito, lina maji mazuri

 

1. Pana jito, lina maji Mazuri,

Yaenda ulimwenguni.

Lametameta nalo Linang’aa.

Walijua jito hilo?

 

Ninakuita nawe njoo!

Utafute jito hilo!

Maji yake yapoza Moyo.

Nawe yateke unywe.

 

2. wanywao maji haya wafurahi,

waimba kwa shangwe kubwa.

Makosa na shida Yanaondoshwa,

Wote waoshwa na Bwana.

Ninakuita nawe njoo …

 

3. Jito hilo latoa maji mengi,

matamu yapendezayo.

Yaponya wagonjwa, Yatia nguvu,

Uchafu watakashika.

Ninakuita nawe njoo …

 

4. maji ya jito hilo ni uzima

unaotoka Kwa Yesu.

Damu yake yenye kiasi kikuu

Imemwagwa tusafike.

Ninakuita nawe njoo …

 

 

142 Babangu kule mbiguni.

 

1. Babangu kule mbinguni,

aliye juu pa malaika,

/:aangalia njia zangu

na kunilinda maisha.:/

 

2. Hata unywele kichwani

hauanguki ovyo tu

/: na siri zote za moyoni

zajulikana kwa Baba.:/

 

3. Zamani nisipojua,

amekwisha kuandika

/:mkononi mwake jina langu,

ndio upedo wake mkuu.:/

 

4. Ee Baba yangu u mwema,

nami nataka kufanya

/:kama malaika wafanyavyo

mbinguni kwako milele!.:/

 

 

143 Nchi nzuri yametameta

 

1. Nchi nzuri yametameta,

Huonekana kule mbali,

Naye Yesu hutuongoza.

Tukafike na sisi huko.

 

/: Sisi mbali, karibu,

Tutaimba na sisi huko!:/

 

2. Kule tutawaona wengi

Wapendwao na Yesu Bwana,

Tutashirikiana nao

Itakuwa furaha kubwa.

Si mbali..

 

3. Tutamwona na Bwana Wetu,

Yesu kristo mwokoai Wetu,

Tutashangilia daima,

Tuna hamu ya kwenda Kwetu.

Si mbali..

 

 

144 Mbele ninaendelea

 

1. Mbele ninaendelea,

Ninazidi kutembea;

Maombi uyasikie,

Ee Bwana, unipandishe.

 

Ee, Bwana, uniinue,

Kwa imani nisimame;

Nipande milima yote,

Ee Bwana,

Unipandishe.

 

2. Sina tamani nikae,

Mahali pa shaka, kamwe;

Hapo wengi wanakaa,

Kuendelea naomba

Ee, Bwana…..

 

3. Nisikae duniani,

Ni mahali pa shetani;

Natazamia mbinguni,

Nitafika na amani.

Ee, Bwana….

 

 

145 Ndoa yetu nzima

 

1. Ndoa yetu nzima

simika, Yesu!

Usiku na mchana

uwepo kwetu.

Leo tuna raha,

Wewe watupa.

/:Ndoa yetu Bwana

ndiwe Baraka!/:

 

2. Atoka kijana,

ataka mchumba

siku zinapita

za kupimana.

Leo twapatana

pamoja kukaa

/:Ndoa yetu…:/

 

3. Vyote hapa chini

vinakaa muda,

vyote vinaoza,

tena vyachakaa.

Pendo la duniani

nalo huchakaa

/:Ndoa yetu…/:

 

4. Kakaa kwetu Bwana,

kutukagua,

pendo letu sisi

lisichakae:

Hivi na tukae

na baraka tu.

/: Ndoa yetu…:/

 

5. Kana arusuni

ulialikwa,

walivyoishiwa

ukaongeza,

nasi shida zetu

utazishinda.

/:Ndoa yetu..:/

 

 

146 Neno la Mungu takata

 

1. Neno la Mungu takata

Lililotoka mbinguni;

Ambalo moto na panga

Haziwezi kulishinda.

Twakushika siku zote

Maishani na kufani.

 

2. Waliotutangulia

Waliokutegemea,

Wamekufa mashujaa;

Nasi tulio watoto.

Twakushika …

 

3. Neno la Mungu takata,

Tukushuhudie nasi

Kwa neno tamu na tendo

Kunako wenzi au adui.

Twakushika …

 

 

147 Tegemea mpaka kufa

 

1. Tegemea mpaka kufa,

Utapata wokovu.

Bwana Yesu ni Mwokozi

Yeye anakupenda.

Uje kwake ‘sikawie’.

Yeye akuokoa.

Njoo upesi! Njoo upesi!

Fika kwa Bwana Yesu.

 

2. Acha mambo ya dunia

Yakuhangaishayo.

Iko mali ya uzima

Unaitiwaa hiyo.

Mali hiyo ni uzima

Utapewa na Bwana.

Njoo upesi! …

 

3. Wakatae, waepuke

Wanaokudanganya;

Na wajinga, wakuponza,

Wakupoteza wewe.

Ila wewe ukatae

Kuondoka kwa Yesu.

Njoo upesi! …

 

4. Ukijua jambo hilo

Usipolifuata

Kosa hilo kubwa sana,

Wapasiwa hukumu.

Vumilia, jizuie

Utapata uzima.

Njoo upesi! …

 

5. Bwana Yesu amekwisha

Kukutengenezea

Kitu chema kwake Mungu,

Ndiko unakokwenda.

Kile kitu upendacho

Kule utakipewa.

Njoo upesi! …

 

 

148 Ondokeni tunaitwa

 

1. Ondokeni! tunaitwa

na walinzi wa juu mnarani

Yerusalemu, amka wee!

Ni usiku wa manane,

yuaja Bwana wa arusi,

wanawali wako wapi?

Amkeni upesi!

Kaziwasheni taa.

Haleluya!

Fuateni arusini

kwenda kumpokea Bwana!

 

2. Sayuni anasikia,

moyo waruka kwa furaha,

yu macho anaondoka.

Mponya wake anashuka

mbinguni mwenye

utukufu,

aleta mwanga wa kweli,

taji yake yaja

na Mwana wa Mungu.

Hosiana!

Twafuata kwenye shangwe

tukale karamu yake.

 

3. Waimbiwa nyimbo nzuri

kwa misemo ya watu wote

na ya malaika mbinguni.

Tukifika mjini kwako

kwenye milango ya malulu

tutakuimbia nasi.

Furaha kama hii

haijasikiwa duniani.

Nasi sasa tunaimba,

tunakusifu, Ee Bwana.

 

 

149 Haya umati wa Yesu

 

1. Haya, umati wa Yesu,

Ulioungwa naye!

Haya, enendeni hima

Katika vita kubwa!

Shetani tayari,

Kupigana na sisi!

 

2. Tumfuate Yesu Kristo,

Tumwamini yeye tu.

Mwovu akituvizia

Sisi hatuogopi.

Majeshi ya mbingu

Ni pamoja na sisi!

 

3. Tukikesha na kuomba

Yesu anayotaka,

Tukishika neno lake

Na kumtegemea

Kwa nguvu hizi tu

Tutaweza kushinda!

 

4. Sasa haya wenzi wangu,

Tumfuate Yesu tu!

Siku za maisha yetu,

Tuwe katika yeye.

Tuache dunia

Kuingia mbinguni!

 

5. Pale Mungu atawapa

Taji walioshinda,

Wapate urithi wao

Nyumbani mwa milele.

Hayani! Tuimbe,

Tumsifu Bwana wetu!

 

 

150 Haya ee moyo wangu

 

1. Haya ee moyo wangu,

imba kwa furaha.

Umwimbie Muumbaji

mbingu na dunia.

Atukuzwaye pote

umsifu na wewe

kwa nguvu zako zote,

umri wako wote.

 

2. Mungu wake Yakobo.

ndiye Mungu wwetu.

Ukimchagua yeye,

una fungu jema,

unacho kitu chema,

umepata mali;

moyo utakung’aa

shida zitakwisha.

 

3. Ni mwenye nguvu nyingi,

hana amshindaye,

kwa hekima aumba

vyote ni ajabu,

misitu na mabonde,

milima,mashamba,

vilivyo baharini

wanyama porini.

 

4. Ana mizungu mingi,

kuponya wanawe.

Anawapa riziki,

hata siku za njaa.

Wenye chakula haba

wanenepa miili:

hata waliofungwa

anawafungua.

 

5. Mashangilio yote

hayamtoshi yeye.

Ni mwema peke yake

nami ni vumbi tu!

Ananihurumia

kwa kuwa ni wake,

kwa hiyo nalikuza

Jina lake pote.

 

 

151 Usiku mtakatifu

 

1. Usiku mtakatifu!

Wengine walala

Wakeshao ni Yosefu tu

na Maria waliomlinda

Yesu mwana mzuri

Yesu mwana mzuri

 

2. Usiku mtakatifu!

Wachunga wapewa

habari nzuri na malaika,

zienezwe popote sasa:

Yesu Mponya kaja

Yesu Mponya kaja.

 

3. Usiku mtakatifu!

Siku ya furaha

imetuangaza Kimungu

tumepewa ukombozi

Kristo amefika

Kristo amefika.

 

 

152 Uliyesulibishwa

 

1. Uliyesulubishwa,

Mtakatifu Bwanangu,

Uwe ngao shidani,

uniombee mimi.

Uliyesulubishwa,

Mtakatifu Bwanangu!

 

2. Wongofu sina hata,

niondolee makosa.

Mwovu akinishtaki

nasumbuka rohoni.

Wongofu sina hata,

niondolee makosa.

 

3. Wewe tu nipokee,

nakukumbilia wee.

Hata nifanye bidii,

nikatoe machozi.

Wewe tu nipokee,

nakukimbilia wewe

 

4. Uwe ngao shidani,

Niombee na mimi!

Hapa nikiumizwa,

Saa ya mwisho ikija:

Uwe ngao shidani,

Niombee na mimi!

 

153 Nimepita  ulimwengu

 

1. Nimepita ulimwengu,

ulimwengu ni mzuri,

lakini natamani

ulimwengu mwingine.

 

2. Nimeona watu wengi,

hutafuta daima

Maisha yao yote,

ndiyo taabu na shida.

 

3. Imebaki hali njema

ya furaha ya roho:

Hubirini popote;

taabu itatulia.

 

4. Msalabani pa Golgota

jerahani mwa Yesu

ni mahali penye raha

kwao wote kabisa.

 

 

154 Bariki yote yawe mema

 

1. Bariki yote yawe mema,

yote yawe mbaraka.

Watu wa nchi za duniani,

uwajaze utukufu.

 

Kaa kwetu, Bwana, bariki.

Uamini wee ee ndugu

kweli yake Kristo.

Jaa utukufu wa Bwana

siku zako zote.

/:Vaa Mwokozi ee

na kweli yake, Haleluya.:/

 

2. Nyumba za wote zibariki

kwa Jina lako takata.

Ujaze utukufu wako,

nchi zote dunia,

Kaa kwetu, Bwana…

 

3. Nyosha mkono ubariki,

waliojiunga nawe.

Wakupokee maishani,

watunzwe nawe milele.

Kaa kwetu, Bwana…..

 

4. Bwana yatunze mambo yote

yaliyo mazuri kwako

Uwape wote wakuombao,

wafanikishe maisha.

Kaa kwetu Bwana….

 

 

155 Hapana rafiki kama Yesu

 

1. Hapana rafiki kama Yesu,

Yu pekee, Yu pekee;

Hapana mpozi kama Yesu

Yu pekee, Yu pekee.

 

Yesu ajua shida zetu,

Aweza kutuongoza;

Hapana rafiki kama Yesu,

Yu pekee yu pekee.

 

2. Yeye anaye sifa, ni Yesu

Yu pekee, yu pekee;

Ndiye aliye mnyenyekevu

Yu pekee, yu pekee;

Yesu ajua……

 

3. Yesu pamoja nasi daima,

Yu pekee, yu pekee;

Kwa usiku aleta salama,

Yu pekee, yu pekee;

Yesu ajua……

 

4. Kulinda Yesu yu Mwaminifu,

Yu pekee, yu pekee;

Atawakubali wahalifu,

Yu pekee, yu pekee;

Yesu ajua…..

 

5. Alipelekwa awe mwokozi,

Yu pekee, yu peee;

Anatutayarisha enzi

Yu pekee, yu pekee;

Yesu ajua…….

 

 

156 Bwana Yesu yuko wapi

 

1. Bwana Yesu yuko wapi,

Mpenzi wangu rafiki?

Njia gani amekwenda?

Nitamwonaje mimi?

Roho yangu yajutishwa

Na dhambi na huzuni;

Yesu mpenzi wangu Mwema

Namtafuta kwa bidii.

 

2. Ninapaza sauti yangu

Nalia:wapi Yesu?

Ndani mwangu sina raha

Mpaka nimwone Yesu.

Ningekuwa na mabawa

Ningeruka upesi

Milimani, mabondeni

Kumtafuta Bwanangu

 

3. Aondoa shida zangu,

Maharibifu yote.

Nikiona taabu mimi

Anituliza yeye.

Nitafanya bidii sana;

Kumtafuta popote;

Sitachoka kutembea

Mchana hata usiku.

 

4. Bwana Yesu nitokee,

Roho inakuita.

Niondoe na maovu

Yesu mwokozi wangu.

Utilize hamu yangu

Kaa kwangu daima.

Nikupende sana wewe,

Niwe wako milele.

 

157 Kijito cha utakaso

 

1. Kijito cha utakaso

ni damu ya Yesu,

Bwana anao uwezo

kunipa wokovu

 

Kijito cha utakaso,

Nizame kuoshwa humo

Namsifu Bwana kwa hiyo

Nimepata utakaso

 

2. Viumbe vipya naona;

damu ina nguvu,

meharibu uovu

ulionidhulumu

 

3. Naondoka kutembea

nuruni mwa mbingu,

Na moyo safi kabisa

kumpendeza Mungu.

 

4. Ni neema ya ajabu

kupakwa na damu;

na Bwana Yesu kumjua

Yesu wa Msalaba.

 

 

158 Aniongoza po pote

 

1. Aniongoza popote

NimwandameSiku zote

Mapenzi yake ni heri

Yalitimizwa kalvari.

 

2. Nitaongozwa na Bwana

Usiku kucha na mchana

Yesu rafiki wa heri

Ninakumbuka kalvari.

 

3. Lanitosha neno lake

Nishikwe na mkono wake

Mapenzi yake ni heri

Yalitimizwa kalvari

 

4. Nitaendelea mbele

Pamoja naye milele

Pendo lake ni hiyari

Bwana Yesu wa Kalvari

 

 

159 Ushirika mkuu, furaha yangu

 

1. Ushirika mkuu, furaha yangu,

Kumtegemea Bwana Yesu,

Nina baraka, amani pia,

Kumtegemea Bwana Yesu.

 

Raha, Raha,

Nina raha na salama,

Raha, Raha,

kwa kumtegemea Yesu.

 

2. Ni halisi kutembea naye,

Kwa kumtegemea Yesu.

Naona nuru njiani mwangu,

Kumtegemea Bwana Yesu.

 

3. Sioni shaka wala hasara,

Kumtegemea Bwana Yesu;

Nina amanikwake Mwolozi,

Kumtegemea Bwana Yesu.

 

 

160 Jioni moyo wangu wakutafuta

 

1. Jioni moyo wangu

wakutafuta Bwana,

na kukushukuru.

Unikazie macho

yenye baraka nyingi,

ung’aze mwili na roho.

 

2. Natumaini tena

rehema yako Baba

hata usiku huu.

Fukuza majaribu

na hila ya shetani,

ukiwa karibu yangu

 

3. Unanipenda sana,

wakaa pamoja nami,

wanikaribisha.

Unanifurahisha

kwa wema wako

mwingi,

sababu hii nakusifu.

 

4. Maisha yanapita upesi,

ni safari ya kwenda

mbinguni.

Unifundishe, Bwana,

kuelekea kwako:

Pazuri ni mbinguni tu.

 

 

161 Usiku uingiapo

 

1. Usiku uingiapo,

umwaze Mungu Mkuu,

aendeshaye dunia

kwa mwendo mtulivu.

 

2. Kwa nini wahangaika

usiku namchana?

Umtwishe huzuni yako

aliyekuumba.

 

3. Kwake haujapunguka

uwezo na msaada.

Atayatimiza yote

aliyoyaanza.

 

4. Ukamwachie kutenda

atakalo kwako!

Kwa hiyo ulale raha

na kufurahiwa.

Comments